-
Amani Kutoka kwa Mungu Wakati Gani?Mnara wa Mlinzi—1986 | Oktoba 1
-
-
19. “Siku ya Yehova” itafyatukaje?
19 “Uharibifu wa ghafula . . . papo kwa hapo,” anasema mtume Paulo. Isaya nabii wa Mungu anaongeza hivi: “Angalia, mashujaa wao wanalia nje, wajumbe wa amani wanalia kwa uchungu.” (Isaya 33:7) Katika mahali pengi, Biblia inaonyesha kwamba Yehova atafikiliza hukumu juu ya mataifa na wanadamu kwa haraka sana, bila kutazamiwa—“kama mwivi usiku.” (1 Wathesalonike 5:2, 3; Yeremia 25:32, 33; Sefania 1:14-18; 2 Petro 3:10) Katika wakati ambao ulimwengu unatangaza kwa sauti kubwa kwamba umefikia usawa fulani wa amani na usalama. “siku ya Yehova” itafyatuka kwa ghafula yenye kugutusha. Watu wa Mungu watakuwa wamelitambua tangazo hilo la “Kuna amani na salama”! Kama lilivyo hasa, nao watakuwa salama katika kimbilio waliloandaliwa na Yehova.—Zaburi 37:39, 40; 46:1, 2; Yoeli 3:16.
-
-
Amani Kutoka kwa Mungu Wakati Gani?Mnara wa Mlinzi—1986 | Oktoba 1
-
-
21. (a) Ni kitendo gani kinachoonyesha mwanzo wa “siku ya Yehova”? (b) “Siku hiyo inasonga mbele kwenye hatua gani kubwa ya mwisho?
21 “Siku ya Yehova” itafyatukaje? Katika usiku huu ambao ndio wenye giza lililo tititi katika historia ya kibinadamu, siku hiyo kwa kweli itakuja “kama mwivi”! Huo ni wakati ambao Mungu atatumia maarifa kuyaongoza mataifa ya mnyama wa UM aigeuke kwa ghafula dini ya uwongo. Kwa kuonyesha chuki ambayo mataifa hayo yamekuwa yakimwonea Babuloni Mkuu kwa njia ya chini chini, yatamfunua wazi aonekane jinsi alivyo hasa na kumharibu kabisa kabisa. Uuaji huo utakuja haraka sana hata waliokuwa hawara wake wa kisiasa wapaaze sauti kwa mshangao wakisema: “Ole! Ole kwa Babuloni, mji maarufu na wenye nguvu! Kwa muda wa saa moja tu adhabu yako imekupata.” Lakini mataifa na majeshi yao yatashambulia watu wa Mungu pia. Halafu, yule Mfalme wa wafalme, Yesu Kristo, atawaharibu adui hao wote na kumwingiza katika shimo refu sana yule mpinzani mkuu, Shetani Ibilisi.—Ufunuo 17:16, 17; 18:10, HNWW; 19:11-21; 20:1-3; linganisha Ezekieli 38:11, 16, 18-23, UV.
-