-
Tunawezaje Kuendelea Kuwa Na‘mtazamo Wa kungojea’?Mnara wa Mlinzi—2013 | Novemba 15
-
-
9-11. Je, unabii ulio katika 1 Wathesalonike 5:3 umetimizwa? Eleza.
9 Soma 1 Wathesalonike 5:1-3. Hivi karibuni, mataifa yatasema, “Amani na usalama!” Hivyo, tunahitaji ‘kukaa macho na kutunza akili zetu’ ili tutambue tangazo hilo. (1 The. 5:6) Ili tuendelee kukaa macho kiroho, acheni tujikumbushe matukio yanayoweka msingi wa kutolewa kwa tangazo hilo muhimu.
10 Baada ya madhara ya vita viwili vya ulimwengu, mataifa yalijitahidi sana kuleta amani. Ushirika wa Mataifa ulianzishwa baada ya vita vya kwanza vya ulimwengu ili kuleta amani. Baada ya vita vya pili vya ulimwengu, watu walitumaini sana Umoja wa Mataifa kuleta amani duniani. Viongozi wa serikali na dini wametumaini kwamba mashirika hayo yatawaletea wanadamu amani. Kwa mfano, Umoja wa Mataifa ulitangaza kwamba mwaka wa 1986 ulikuwa Mwaka wa Amani Ulimwenguni. Mwaka huo, viongozi wa serikali na dini kutoka mataifa mengi walikutana huko Assisi, nchini Italia pamoja na kiongozi wa Kanisa Katoliki ili kuombea amani.
11 Hata hivyo, tangazo hilo la amani na usalama au tangazo lingine lolote kama hilo halijatimiza unabii ulio katika 1 Wathesalonike 5:3. Kwa nini? Kwa sababu “uharibifu wa ghafula” uliotabiriwa bado haujatokea.
12. Tunajua nini kuhusu tangazo la “Amani na usalama”?
12 Ni nani atakayetoa tangazo hilo muhimu la “Amani na usalama”? Viongozi wa dini zinazodai kuwa za Kikristo na wa dini nyingine watahusikaje katika jambo hilo? Viongozi wa serikali mbalimbali watahusika namna gani katika tangazo hilo? Maandiko hayatuelezi. Hata hivyo, tunajua kwamba tangazo hilo halitakuwa la kweli hata likitolewa na nani au kwa njia yenye kusadikisha kadiri gani. Mfumo huu wa kale wa mambo utaendelea kuongozwa na Shetani. Umezorota kabisa na utaendelea kuwa hivyo. Litakuwa jambo la kusikitisha kama nini ikiwa tutaamini propaganda za Shetani na kuvunja msimamo wetu wa Kikristo wa kutounga mkono upande wowote!
-
-
Tunawezaje Kuendelea Kuwa Na‘mtazamo Wa kungojea’?Mnara wa Mlinzi—2013 | Novemba 15
-
-
14. Ni nini kinachoonyesha kwamba Babiloni Mkubwa ataharibiwa karibuni?
14 Babiloni Mkubwa, yaani, milki ya ulimwenguni pote ya dini ya uwongo itaharibiwa kama inavyostahili. “Vikundi vya watu na umati na mataifa na lugha” havitaweza kumsaidia. Tayari tunaona dalili zinazoonyesha kwamba mwisho wake unakaribia. (Ufu. 16:12; 17:15-18; 18:7, 8, 21) Kwa kweli, leo vyombo vya habari vinaonyesha kwamba watu wengi hawaungi mkono dini na viongozi wa kidini, badala yake wanazidi kuwashutumu. Hata hivyo, viongozi wa Babiloni Mkubwa hawatambui kwamba wako hatarini. Wamekosea kama nini! Baada ya tangazo la “Amani na usalama!” sehemu za kisiasa za mfumo wa Shetani zitageukia ghafla dini ya uwongo na kuiharibu kabisa. Babiloni Mkubwa hataonekana tena kamwe! Kwa kweli, ni muhimu kungojea kwa subira matukio hayo ya pekee.—Ufu. 18:8, 10.
-