-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—1999 | Julai 15
-
-
“Sasa tunawapa nyinyi maagizo, akina ndugu, . . . kujiondoa kutoka kwa kila ndugu anayetembea bila utaratibu na si kulingana na mapokeo mliyopokea kutoka kwetu. Kwa upande wenu, akina ndugu, msikate tamaa katika kutenda lililo sawa. Lakini ikiwa yeyote hawi mtiifu kwa neno letu kupitia barua hii, mfulize kumtia mtu huyu alama, komeni kushirikiana naye, ili apate kuaibika. Na bado msiwe mkimwona yeye kuwa adui, bali endeleeni kumwonya kwa upole kama ndugu.”—2 Wathesalonike 3:6, 13-15.
-
-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—1999 | Julai 15
-
-
Hali inayohusisha watu “wasio na utaratibu” ambayo inazungumziwa katika 2 Wathesalonike yatofautiana na hali tatu zilizo juu. Paulo aliandika kwamba hao bado walikuwa “ndugu,” waliopasa kuonywa kwa upole na kutendewa kama ndugu. Kwa hiyo, tatizo la ndugu hao “wasio na utaratibu” halikuwa jambo la kibinafsi kati ya Wakristo wala halikuwa zito vya kutosha hivi kwamba wazee wa kutaniko walipaswa kuchukua hatua ya kutenga na ushirika, kama vile ambavyo Paulo alifanya kuhusu ile hali ya ukosefu wa adili huko Korintho. Watu “wasio na utaratibu” hawakuwa na hatia ya dhambi nzito, kama yule mtu aliyetengwa na ushirika huko Korintho.
-
-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—1999 | Julai 15
-
-
Pia alilijulisha kutaniko kwamba ingefaa wao wenyewe wakiwa Wakristo mmoja-mmoja ‘watie alama’ watu wasio na utaratibu. Hilo lilimaanisha kwamba watu mmoja-mmoja wapaswa kutambua watu ambao matendo yao yalilingana na mwendo ambao kutaniko lilikuwa limetahadharishwa dhidi yake waziwazi. Paulo aliwashauri ‘wajiondoe kutoka kwa kila ndugu anayetembea bila utaratibu.’ Bila shaka hilo halingemaanisha kumwepuka kabisa mtu huyo, kwa kuwa bado walipaswa ‘kuendelea kumwonya kwa upole kama ndugu.’ Wangeendelea kuwa na ushirikiano wa Kikristo naye kwenye mikutano na labda kwenye huduma. Wangeweza kutumaini kwamba ndugu yao angeitikia onyo la upole na kuacha njia zake zenye kusumbua.
-