Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Waangalizi Wanaochunga Kundi
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • 9 Wale ambao wana sifa za kustahili kuwa waangalizi wanatenda kwa hekima katika maisha yao. Ikiwa amefunga ndoa, mwangalizi anapaswa kuishi kupatana na viwango vya Kikristo kuhusu ndoa, yaani, awe mume wa mke mmoja na anayeisimamia nyumba yake vizuri. Ikiwa mwangalizi ana watoto wanaoamini ambao wanajitiisha na kuchukua mambo kwa uzito na hawana mashtaka ya kuwa wapotovu au waasi, ndugu na dada kutanikoni wanaweza kumtumaini na kumwomba ushauri kuhusu familia na maisha ya Kikristo. Pia, mwangalizi ni mtu asiyelaumika na hapaswi kuwa na shtaka na awe mwenye kushuhudiwa vema hata na watu walio nje. Hana mashtaka yoyote kwa sababu ya mwenendo usiofaa ambao unaweza kuharibu sifa nzuri ya kutaniko. Si mtu ambaye amekaripiwa hivi karibuni kwa sababu ya kosa zito. Wengine kutanikoni wanachochewa kuiga mfano wake mzuri na wana hakika kwamba mwangalizi huyo atahangaikia hali yao ya kiroho.—1 Kor. 11:1; 16:15, 16.

      10 Wanaume hao wanaostahili wanalitumikia kutaniko la Kikristo kama walivyofanya wale wanaume wazee wa Israeli waliotajwa kuwa “wenye hekima na busara na wenye uzoefu.” (Kum. 1:13) Haimaanishi kwamba wazee Wakristo ni wakamilifu, lakini wanajulikana kutanikoni na katika jamii kuwa wanaume waaminifu na wenye kumwogopa Mungu ambao maisha yao yameonyesha kwamba wamekuwa wakiishi kupatana na kanuni za Mungu. Kwa sababu ya kuwa wasiolaumika, wana uhuru wa kusema kutanikoni.—Rom. 3:23.

  • Waangalizi Wanaochunga Kundi
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • 11 Wanaume wanaostahili kuwa waangalizi wanaonyesha kiasi katika mazoea na wanaposhughulika na wengine. Hawapaswi kuwa washupavu. Badala yake, wanapaswa kuwa na usawaziko na wanaojidhibiti. Wanapaswa kuwa na kiasi katika kula, kunywa, tafrija, mambo wanayopenda, na burudani. Wanakunywa pombe kwa kiasi ili wasishtakiwe kwa madai ya ulevi au wasiwe na shtaka la kuwa walevi. Mtu ambaye hisi zake zimepumbazwa na pombe hushindwa kujidhibiti, naye hawezi kushughulikia mahitaji ya kiroho ya kutaniko.

      12 Ili kusimamia kutaniko inafaa mtu awe mwenye utaratibu. Tabia yake njema inaonekana wazi katika mwonekano wake, nyumbani kwake, na katika shughuli zake za kila siku. Mtu wa namna hiyo huepuka kuahirisha mambo; anaona kinachohitajiwa na kuchukua hatua mara moja. Anashikamana na kanuni za Biblia.

  • Waangalizi Wanaochunga Kundi
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • 14 Pia, yule anayestahili kutumikia akiwa mwangalizi kutanikoni anapaswa kuwa mwenye utimamu wa akili. Hilo linamaanisha awe mtulivu, na asiyefanya uamuzi haraka-haraka. Anazijua vizuri kanuni za Yehova na jinsi zinavyotumika. Mtu mwenye utimamu wa akili yuko tayari kukubali ushauri na mwongozo. Yeye si mnafiki.

  • Waangalizi Wanaochunga Kundi
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • 15 Paulo alimkumbusha Tito kwamba mwangalizi ni mtu anayependa mema. Anapaswa kuwa mwadilifu na mshikamanifu. Sifa hizo zitaonekana anaposhughulika na wengine na anapotetea kwa uthabiti yale yaliyo sawa na yaliyo mema. Hayumbi-yumbi katika ujitoaji wake kwa Yehova naye daima hufuata kanuni za uadilifu. Anaweza kutunza siri. Pia, ni mkaribishaji wageni, yuko tayari kujitolea yeye mwenyewe na mali yake ili kuwanufaisha wengine.—Mdo. 20:33-35.

      16 Ili awe mwangalizi mzuri, anapaswa kuwa mwenye uwezo wa kufundisha. Kulingana na maneno ya Paulo kwa Tito, mwangalizi anapaswa kuwa “anayefuata kikamili neno la uaminifu katika ustadi wake wa kufundisha, ili aweze kutia moyo kwa fundisho lenye manufaa na pia kuwakaripia wale ambao hulipinga.” (Tito 1:9) Ana uwezo wa kujadiliana, kuthibitisha, kushinda vipingamizi, na kutumia Maandiko kwa njia itakayowasadikisha wengine na kuimarisha imani yao. Mwangalizi anatumia uwezo huo wa kufundisha katika nyakati zinazofaa na katika nyakati ngumu. (2 Tim. 4:2) Anahitaji kuwa na subira ili aweze kumkaripia kwa upole mtu aliyekosea au kumsadikisha mtu mwenye shaka na kumchochea afanye mambo mazuri kwa imani. Kuwa na uwezo wa kufundisha watu wengi au mtu mmoja-mmoja kunaonyesha kwamba mwangalizi anatimiza sifa hiyo muhimu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki