-
Yehova AtakutegemezaMnara wa Mlinzi—2015 | Desemba 15
-
-
13. Tunapaswa kuwa na maoni gani kuhusu mapendekezo ya kitiba?
13 Leo, Mkristo mwenzetu hawezi kutumia “zawadi za maponyo” ili kutuponya kimuujiza. Hata hivyo, baadhi ya akina ndugu wenye nia nzuri, huwapendekezea wengine matibabu fulani hata bila kuombwa ushauri. Ni kweli kwamba wengine huenda wakatoa mapendekezo mazuri. Kwa mfano, Paulo alifanya hivyo Timotheo alipokuwa na matatizo ya tumbo ambayo huenda yalisababishwa na kunywa maji yasiyo safi.a (Soma 1 Timotheo 5:23.) Lakini jambo hilo ni tofauti kabisa na kujaribu kumshawishi Mkristo mwenzetu atumie mitishamba, tiba, au lishe fulani ambayo huenda isiwe na matokeo mazuri au katika visa fulani inaweza kusababisha madhara. Nyakati nyingine, watu fulani hujaribu kuwashawishi wengine kwa kusema hivi: ‘Ndugu yangu wa ukoo aliugua ugonjwa huohuo, na baada ya kutumia . . . alipona kabisa.’ Hata ikiwa pendekezo hilo linaonekana kuwa linafaa, ni vizuri tukumbuke kwamba hata dawa na tiba zinazotumiwa na watu wengi zinaweza kuwa hatari.—Soma Methali 27:12.
-
-
Yehova AtakutegemezaMnara wa Mlinzi—2015 | Desemba 15
-
-
a Kitabu kimoja kinasema hivi: “Imethibitishwa kisayansi kwamba vijidudu vya homa ya matumbo na vijidudu vingine hatari hufa mara moja vinapochanganywa na divai.”—The Origins and Ancient History of Wine.
-