Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kufanikiwa kwa Gharama Yoyote?
    Mnara wa Mlinzi—1988 | Agosti 15
    • Kwa kuwa umaskini ni tele, watu wengi wamefuatia mafanikio ya kipesa kwa kusahaulia mbali kila kitu kinginecho. Watu fulani wanageukia kutofuata haki ili watimize jambo hilo. Ingawa hivyo, wanapokuwa Wakristo wa kweli, inawapasa wawe wamekwisha kuuacha nyuma daima mwelekeo huu ili kujipatanisha na viwango vyenye uadilifu vya Biblia.

      Hata hivyo, hata Wakristo fulani wananasika tena katika kulenga shabaha kwenye miradi ya kilimwengu. Huenda wao wakaanguka ndani ya mwenendo usio wa Kikristo ili wafikie mafanikio. Wazazi wanaachilia jamaa zao bila kuzijali. Watu mmoja mmoja wanakosa kujali utumishi wao kwa Mungu. Je! wewe unafikiri tokeo lingekuwa nini kuhusiana na kupata utoshelevu na furaha maishani?

      Ikitutia chonjo juu ya tokeo lenyewe, Biblia inaonya hivi: “Wale ambao wamepiga moyo konde wawe matajiri wanaanguka katika kishawishi na kitanzi na tamaa nyingi zisizo za akili na zenye kujaa maumizo . . . Kwa maana upendo wa pesa ni mzizi wa namna zote za mambo yenye kudhuru, na kwa kujitahidi kufikia upendo huo watu fulani wamepotezwa njia kutoka kwenye imani na wamejichoma-choma wenyewe mwili wote kwa maumivu mengi.”​—1 Timotheo 6:9, 10, NW.

  • Kufanikiwa kwa Gharama Yoyote?
    Mnara wa Mlinzi—1988 | Agosti 15
    • Upendo wa mali ni bwana-mkubwa mwenye kudai-dai. Huo unawatoza watu wakati, imara, na uwezo mbalimbali; na unakaba roho ya bidii ya kujitolea Mungu na kuitoa. Kwa kawaida unashawishi-shawishi watu watafute utajiri ulio mkubwa hata zaidi na fahari ya kilimwengu, hivyo ukiwavuta hata zaidi kutoka kwenye ile imani. Biblia inasema hivi kwa kufaa: “Mpendaji tu wa fedha hatatosheka na fedha, wala mpendaji ye yote wa utajiri atosheke na mapato.”​—Mhubiri 5:10, NW.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki