Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tofauti Kati ya Watu Wanaomtumikia Yehova na Wasiomtumikia
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2018 | Januari
    • 3. Orodha ya sifa zinazotajwa kwenye 2 Timotheo 3:2-5 inawahusu nani?

      3 Mtume Paulo alisema kwamba “siku za mwisho” zingetokeza “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.” Kisha aliorodhesha sifa 19 zisizofaa ambazo watu wangekuwa nazo katika kipindi hicho. Orodha hiyo ni sawa na ile inayopatikana katika Waroma 1:29-31. Hata hivyo, orodha ambayo Paulo aliandika kwenye barua yake kwa Timotheo inatia ndani mambo ambayo hayatajwi mahali pengine popote katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Katika orodha hiyo, Paulo anaanza kwa kusema maneno haya: “Kwa maana watu watakuwa . . . ” Hata hivyo, si watu wote walio na tabia kama hizo. Wakristo wanaonyesha sifa tofauti kabisa.—Soma Malaki 3:18.

  • Tofauti Kati ya Watu Wanaomtumikia Yehova na Wasiomtumikia
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2018 | Januari
    • 4. Ungewafafanuaje watu waliojaa kiburi?

      4 Baada ya kutaja kwamba watu wengi wangekuwa wenye kujipenda wenyewe na wenye kupenda pesa, Paulo aliandika pia kwamba watu wangekuwa wenye kujidai, wenye majivuno, na waliojaa kiburi, tabia zinazodhihirisha mtazamo wa kujiona kuwa bora kwa sababu ya uwezo, sura, utajiri, au cheo. Watu wenye tabia kama hizo hutamani sana wasifiwe-sifiwe na kuonwa kuwa wa pekee. Msomi mmoja aliandika hivi kumhusu mtu aliyejaa kiburi: “Moyoni mwake ana madhabahu ndogo ambapo yeye mwenyewe hupiga magoti ili kujiinamia.” Baadhi ya watu wamesema kwamba kiburi kinachukiza sana hivi kwamba hata watu wenye kiburi huchukizwa na watu wenye kiburi.

  • Tofauti Kati ya Watu Wanaomtumikia Yehova na Wasiomtumikia
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2018 | Januari
    • 8. (a) Baadhi ya watu leo wana maoni gani kuhusu kuwatii wazazi? (b) Maandiko yanawatia moyo watoto wafanye nini?

      8 Paulo alieleza jinsi ambavyo watu wa siku za mwisho wangewatendea wengine. Aliandika kwamba katika siku za mwisho watoto hawangewatii wazazi wao. Ingawa nyakati nyingine tabia hiyo inakubalika na kuungwa mkono kwenye vitabu, sinema, na vipindi vya televisheni, kutotii hufanya umoja uliopo katika familia, ambayo ndiyo msingi wa jamii, udhoofike. Kwa muda mrefu watu wametambua ukweli huo. Katika milki ya kale ya Ugiriki, mwanamume aliyempiga mzazi wake, alipoteza haki zake zote za kiraia; chini ya sheria za Roma, kitendo cha mtu kumpiga baba yake kilionwa kuwa sawa na kuua. Maandiko ya Kiebrania na Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo huwatia moyo watoto wawaheshimu wazazi wao.—Kut. 20:12; Efe. 6:1-3.

  • Tofauti Kati ya Watu Wanaomtumikia Yehova na Wasiomtumikia
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2018 | Januari
    • 10, 11. (a) Ni sifa gani mbaya ambazo zingeonyesha kwamba watu hawana upendo? (b) Wakristo wa kweli wanawapenda wanadamu wenzao kwa kadiri gani?

      10 Paulo aliorodhesha sifa nyingine zinazoonyesha kwamba watu hawangewapenda wengine. Haishangazi anataja kwamba watu wangekuwa wasio na shukrani baada ya kusema kwamba watoto wangekuwa “wasiotii wazazi,” kwani, mtazamo wa kukosa shukrani huonyeshwa na watu ambao hawathamini fadhili ambazo wengine wanawaonyesha. Pia, watu wangekosa ushikamanifu. Nao hawangetaka makubaliano yoyote; wangeonyesha kwamba hawana nia ya kupatana na wengine. Wangekuwa wakufuru na wasaliti, wakiwatukana wanadamu wenzao na hata Mungu mwenyewe. Pia, kungekuwa na wachongezi, yaani, watu ambao wangesema mambo yaliyokusudiwa kuwaharibia wengine sifa.a

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki