-
Je, Biblia Ilitabiri Mitazamo na Matendo ya Watu Leo?Maswali ya Biblia Yajibiwa
-
-
Leo, unabii huo umetimizwa kwa kuwa watu wa siku hizi wanajifikiria kupita kiasi, wanajitanguliza, wanafikiria zaidi kujitosheleza, kujipendeza, na mambo kama hayo yanayowafanya wajihisi wana kusudi maishani. Tabia hizo ni za kawaida sana siku hizi hivi kwamba kuna vikundi vya watu wanaoitwa Kizazi cha Mimi Kwanza. Watu wengi wanajipenda sana wenyewe hivi kwamba ‘hawapendi wema,’ yaani, hawana uwezo wa kupenda sifa nzuri. Wamekuwa “wasio na shukrani,” hivi kwamba hawaoni umuhimu wa kuonyesha shukrani kwa ajili ya vitu walivyo navyo au mambo ambayo watu wengine wanawafanyia.—2 Timotheo 3:2, 3.
-
-
Je, Biblia Ilitabiri Mitazamo na Matendo ya Watu Leo?Maswali ya Biblia Yajibiwa
-
-
Uchongezi. “Wakufuru” na “wachongezi” wanapatikana kila mahali. (2 Timotheo 3:2, 3) Maneno hayo yanarejelea wale wanaowadhihaki watu wengine au kumdhihaki Mungu au wanaosema uwongo kuwahusu.
Ukaidi. Watu wengi ‘si washikamanifu,’ ‘hawataki makubaliano yoyote,’ “wasaliti,” na “wenye vichwa vigumu.” (2 Timotheo 3:2-4) Wanaonyesha sifa hizo mbaya kwa kukataa kusikiliza maoni ya wengine, kusuluhisha mambo, au kutimiza ahadi walizoweka awali.
Jeuri. Watu wengi leo ni “wakali,” wasiozuia hasira, na mara nyingi wanawatendea wengine kwa ukatili sana.—2 Timotheo 3:3.
-
-
Je, Biblia Ilitabiri Mitazamo na Matendo ya Watu Leo?Maswali ya Biblia Yajibiwa
-
-
Kukosa upendo katika familia. Wale “wasiotii wazazi” na “wasio na upendo wa asili [katika familia]” wamefanya kuwe na ongezeko la watu wasiotunza familia zao, wanaowatenda vibaya na kwa ukatili watu wa familia.—2 Timotheo 3:2, 3.
-