Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tofauti Kati ya Watu Wanaomtumikia Yehova na Wasiomtumikia
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2018 | Januari
    • 9. Ni nini kitakachowasaidia watoto wawatii wazazi wao?

      9 Watoto wanaweza kujilinda wasiathiriwe na roho ya kutotii kwa kutafakari mambo ambayo wazazi wao wamewatendea. Watachochewa kuthamini mambo hayo ikiwa wataelewa kwamba utii ni takwa la Mungu ambaye ndiye Baba yetu sote. Watoto wanaposema mambo mazuri kuwahusu wazazi wao, wanaweza kuwachochea vijana wengine waanze kuwa na maoni mazuri kuwahusu wazazi wao pia. Bila shaka, ikiwa wazazi hawana upendo wa asili kuelekea watoto wao, huenda ikawa vigumu kwa watoto kuwatii kutoka moyoni. Kwa upande mwingine, mtoto anapohisi kwamba wazazi wake wanampenda kikweli, atachochewa kuwatii hata anaposhawishiwa kutotii. Austin anakiri hivi: “Ingawa nyakati nyingine nilishawishika kufanya mambo niliyokatazwa na wazazi wangu, walinipa miongozo ambayo haikunibana, walinieleza sababu ya sheria walizotoa, na kuzungumza nami kwa uhuru. Mambo hayo yalinisaidia niwe mtiifu. Niliona kwamba wananijali na hilo lilinichochea nitamani kuwafurahisha.”

      10, 11. (a) Ni sifa gani mbaya ambazo zingeonyesha kwamba watu hawana upendo? (b) Wakristo wa kweli wanawapenda wanadamu wenzao kwa kadiri gani?

      10 Paulo aliorodhesha sifa nyingine zinazoonyesha kwamba watu hawangewapenda wengine. Haishangazi anataja kwamba watu wangekuwa wasio na shukrani baada ya kusema kwamba watoto wangekuwa “wasiotii wazazi,” kwani, mtazamo wa kukosa shukrani huonyeshwa na watu ambao hawathamini fadhili ambazo wengine wanawaonyesha. Pia, watu wangekosa ushikamanifu. Nao hawangetaka makubaliano yoyote; wangeonyesha kwamba hawana nia ya kupatana na wengine. Wangekuwa wakufuru na wasaliti, wakiwatukana wanadamu wenzao na hata Mungu mwenyewe. Pia, kungekuwa na wachongezi, yaani, watu ambao wangesema mambo yaliyokusudiwa kuwaharibia wengine sifa.a

  • Tofauti Kati ya Watu Wanaomtumikia Yehova na Wasiomtumikia
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2018 | Januari
    • a Neno “mchongezi” au “mshtaki” katika Kigiriki ni di·aʹbo·los, nalo linatumiwa katika Biblia kumrejelea Shetani, yule mchongezi mwovu wa Mungu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki