-
Wazazi—Wasaidieni Watoto Wenu Wawe ‘Wenye Hekima kwa Ajili ya Wokovu’Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2017 | Desemba
-
-
3. (a) Timotheo alijifunzaje Ukristo, naye aliitikiaje mafundisho hayo? (b) Paulo alimhimiza Timotheo kuhusu mambo gani matatu yanayohusika katika kujifunza?
3 Huenda Timotheo alianza kufundishwa mafundisho ya Kikristo mwaka wa 47 W.K. mtume Paulo alipotembelea jiji la Listra kwa mara ya kwanza. Ingawa huenda wakati huo Timotheo alikuwa kijana, inaonekana kwamba alikuwa akifanya maendeleo ya kiroho. Kisha baada ya miaka miwili, akaanza kusafiri na Paulo. Miaka 16 hivi baadaye, Paulo alimwandikia hivi Timotheo: “Endelea katika mambo uliyojifunza na uliyoshawishiwa kuamini, ukijua ni kutoka kwa watu gani ulijifunza hayo na kwamba tangu utoto mchanga umeyajua maandishi matakatifu [Maandiko ya Kiebrania], ambayo yanaweza kukufanya uwe mwenye hekima kwa ajili ya wokovu kupitia imani kuhusiana na Kristo Yesu.” (2 Tim. 3:14, 15) Ona kwamba Paulo anataja (1) kuyajua maandishi matakatifu, (2) kushawishiwa kuamini mambo uliyojifunza, na (3) kuwa na hekima kwa ajili ya wokovu kupitia imani kuhusiana na Kristo Yesu.
-
-
Wazazi—Wasaidieni Watoto Wenu Wawe ‘Wenye Hekima kwa Ajili ya Wokovu’Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2017 | Desemba
-
-
“ULIYOSHAWISHIWA KUAMINI”
5. (a) Maneno “kushawishiwa kuamini” yanamaanisha nini? (b) Tunajuaje kwamba Timotheo alishawishiwa kuamini habari njema kumhusu Yesu?
5 Kuwa na ujuzi wa maandishi matakatifu ni muhimu. Hata hivyo, mengi zaidi yanahusika katika kuwasaidia watoto wako wawe na elimu ya kiroho kuliko kuwafundisha tu kuhusu watu na matukio yanayosimuliwa katika Biblia. Timotheo pia ‘alishawishiwa kuamini.’ Katika lugha ya awali, maneno hayo yanamaanisha “kuhakikishiwa” au “kusadikishwa na kuwa na uhakika kuhusiana na ukweli wa jambo fulani.” Timotheo aliyajua Maandiko ya Kiebrania tangu alipokuwa mtoto mchanga. Lakini baadaye alisadikishwa kupitia uthibitisho ulio hakika kwamba Yesu alikuwa Masihi. Kwa maneno mengine, ujuzi aliokuwa nao ulitegemezwa na mambo hakika aliyosadiki. Kwa kweli, usadikisho ambao Timotheo alikuwa nao kuhusu habari njema ulikuwa wenye nguvu sana hivi kwamba akabatizwa na kujiunga na Paulo katika kazi ya umishonari.
6. Unaweza kuwasaidiaje watoto wako washawishiwe kuamini mambo wanayojifunza katika Neno la Mungu?
6 Unaweza kuwasaidiaje watoto wako wawe na usadikisho utakaowafanya washawishiwe kuamini, kama ilivyokuwa kwa Timotheo? Kwanza, uwe na subira. Usadikisho hauji kwa siku moja; wala mtoto hawezi kurithi usadikisho kutoka kwako eti kwa sababu wewe umeshawishiwa kuamini. Kila mtoto anahitaji kutumia ‘nguvu zake za kufikiri’ ili asitawishe usadikisho kuhusu kweli za Biblia. (Soma Waroma 12:1.) Ukiwa mzazi, una jukumu muhimu la kumsaidia mtoto wako asitawishe usadikisho, hasa anapouliza maswali. Fikiria mfano ufuatao.
7, 8. (a) Baba mmoja Mkristo anaonyeshaje subira anapomfundisha binti yake? (b) Ni nyakati zipi ulipohisi kwamba unahitaji kuwa mwenye subira unapomfundisha mtoto wako?
7 Thomas, baba mwenye binti aliye na umri wa miaka 11, anaeleza hivi: “Binti yangu anaweza kuniuliza hivi, ‛Je, inawezekana Yehova alitumia mageuzi kuanzisha uhai duniani?’ au, ‛Kwa nini hatujihusishi na mambo ya kijamii kama vile kupiga kura ili kuboresha mambo?’ Nyakati nyingine ninalazimika kujizuia ili nisimwambie tu mambo anayopaswa kuamini. Ukweli ni kwamba usadikisho hautokani na kujua tu habari nyingi kuhusu kweli. Unatokana na kujifunza mambo madogo-madogo yenye kusadikisha.”
8 Kama ambavyo Thomas amejifunza, kufundisha kunahitaji subira. Kwa kweli, sifa ya subira ni muhimu kwa Wakristo wote. (Kol. 3:12) Thomas anatambua kwamba huenda akahitaji kuendelea kuwa na mazungumzo ya mara kwa mara pamoja na binti yake kwa kipindi kirefu. Anahitaji kutoa sababu za Kimaandiko ili binti yake asitawishe usadikisho kuhusu mambo anayojifunza. Thomas anasema hivi: “Mimi na mke wangu hutaka kujua ikiwa kwa kweli binti yetu anaamini mambo anayojifunza na ikiwa anakubaliana na mambo hayo. Tunafurahi anapouliza maswali. Kwa kweli, ningekuwa na wasiwasi ikiwa angekubaliana tu na jambo fulani bila kuuliza maswali.”
9. Unaweza kufanya nini ili kukazia Neno la Mungu akilini na moyoni mwa watoto wako?
9 Wazazi wanapowafundisha watoto wao kwa subira, hatua kwa hatua watoto wao wataanza kuelewa “upana na urefu na kimo na kina” cha imani. (Efe. 3:18) Tunaweza kutafuta habari zinazowafaa kulingana na umri na uwezo wao. Kadiri wanavyosadiki mambo wanayojifunza, ndivyo watakavyokuwa tayari kutetea imani yao mbele ya wengine, kutia ndani wanafunzi wenzao. (1 Pet. 3:15) Kwa mfano, je, watoto wako wanaweza kutumia Biblia kueleza kinachotokea mtu anapokufa? Je, wanakubaliana na yale ambayo Biblia inasema?a Naam, kukazia Neno la Mungu akilini na moyoni mwa mtoto wako kunahitaji subira, hata hivyo, jitihada zako si za bure.—Kum. 6:6, 7.
10. Ni jambo gani linalopaswa kuwa sehemu muhimu ya ufundishaji wako?
10 Bila shaka, mfano unaowawekea watoto wako ni muhimu sana ili kuwasaidia wawe na usadikisho. Stephanie, mama mwenye mabinti watatu, anasema hivi: “Tangu watoto wangu walipokuwa wachanga, nimejiuliza, ‘Je, mimi huwaeleza watoto wangu kwa nini mimi ninasadiki kwamba Yehova yupo, ananipenda, na kwamba njia zake ni za uadilifu? Je, watoto wangu wanaona waziwazi kwamba mimi ninampenda Yehova kutoka moyoni?’ Siwezi kutarajia watoto wangu washawishiwe kuamini ilhali mimi sijashawishiwa kuamini.”
-