Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Eunike na Loisi—Waelimishaji Walio Vielelezo Bora
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Mei 15
    • Hata hivyo, Eunike hakuwa peke yake katika itikadi zake. Yaonekana kwamba Timotheo alipokea maagizo katika “maandishi matakatifu” kutoka kwa mama yake na kutoka kwa nyanya yake wa upande wa mama, Loisi.a Mtume Paulo alimhimiza sana Timotheo hivi: “Endelea katika mambo uliyojifunza na uliyoshawishwa kuamini, ukijua ni kutoka kwa watu gani ulijifunza hayo na kwamba tangu utoto sana umeyajua maandishi matakatifu, yawezayo kukufanya uwe mwenye hekima kwa ajili ya wokovu kupitia imani kuhusiana na Kristo Yesu.”—2 Timotheo 3:14, 15.

  • Eunike na Loisi—Waelimishaji Walio Vielelezo Bora
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Mei 15
    • Timotheo ‘alishawishwa kuamini’ kweli za Maandiko. Kulingana na kamusi moja ya Kigiriki, neno alilotumia Paulo hapa humaanisha “kushawishiwa kwa uthabiti; kuhakikishiwa” kitu fulani. Bila shaka, wakati na jitihada kubwa zilihitajiwa ili kukaza usadikisho huo ndani ya moyo wa Timotheo, ukimsaidia kusababu juu ya Neno la Mungu na kudhihirisha imani katika hilo. Basi, yaonekana kwamba, Eunike na Loisi pia walifanya bidii kumfundisha Timotheo Maandiko. Nao wanawake hao wenye kumhofu Mungu walivuna thawabu iliyoje! Paulo aliweza kuandika hivi juu ya Timotheo: “Nakumbuka imani iliyo katika wewe isiyo na unafiki wowote, na iliyokaa kwanza katika nyanya yako Loisi na mama yako Eunike, lakini ambayo mimi nina hakika imo pia katika wewe.”—2 Timotheo 1:5.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki