Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Biblia Inawezaje Kukusaidia?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • Somo la 1. Biblia.

      SOMO LA 01

      Biblia Inawezaje Kukusaidia?

      Sisi sote hujiuliza maswali kuhusu maisha, kuteseka, kifo, na wakati ujao. Pia tunahangaikia shughuli za kila siku, kama vile kupata riziki na jinsi ya kuwa na familia yenye furaha. Watu wengi wametambua kwamba Biblia imewasaidia kupata majibu ya maswali muhimu maishani na pia ushauri unaotegemeka kuhusu maisha ya kila siku. Je, unamjua mtu yeyote ambaye anaweza kunufaika kwa kujifunza Biblia?

      1. Biblia inajibu maswali gani?

      Biblia inajibu maswali haya muhimu: Uhai ulianzaje? Maisha yana kusudi gani? Kwa nini watu huteseka? Ni nini humpata mtu anapokufa? Ingawa kila mtu anapenda amani, kwa nini kuna vita ulimwenguni? Ni nini kitakachoipata dunia wakati ujao? Biblia inatutia moyo tutafute majibu ya maswali hayo, na watu wengi wamepata majibu yenye kuridhisha.

      2. Biblia inawezaje kutusaidia tufurahie maisha ya kila siku?

      Biblia hutupatia ushauri mzuri. Kwa mfano, inatufundisha jinsi ya kuwa na familia yenye furaha. Pia, inatoa ushauri kuhusu kukabiliana na mikazo na jinsi ya kufurahia kazi. Utajifunza yale ambayo Biblia inafundisha kuhusu mambo hayo na mengine mengi katika chapisho hili. Tuna hakika utakubali kwamba “kila Andiko [katika Biblia] . . . ni lenye faida.”​—2 Timotheo 3:16.

      Chapisho hili si Biblia. Hata hivyo, litakusaidia kuichunguza Biblia. Kwa hiyo, tunakutia moyo usome maandiko yaliyo kwenye masomo haya na uyalinganishe na mambo unayojifunza.

      CHIMBA ZAIDI

      Jifunze jinsi ambavyo Biblia imewasaidia watu, jinsi unavyoweza kufurahia kuisoma, na kwa nini unapaswa kutafuta msaada ili kuielewa.

      3. Biblia inaweza kutuongoza

      Biblia ni kama tochi yenye mwangaza mkali. Tunaweza kutumia Biblia kujua jinsi ya kufanya maamuzi mazuri na kutambua mambo yatakayotokea wakati ujao.

      Soma Zaburi 119:105, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Yule aliyeandika andiko hili alikuwa na maoni gani kuhusu Biblia?

      • Wewe una maoni gani kuhusu Biblia?

      Mwanamume akitembea gizani kwenye ufuo wenye mawe, anatumia tochi kumulika njia yake.

      4. Biblia inajibu maswali tunayojiuliza

      Mwanamke fulani alitambua kwamba Biblia ina majibu ya maswali yaliyomhangaisha kwa miaka mingi. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali haya:

      VIDEO: Usikate Tamaa Kamwe! (1:48)

      • Katika video hiyo, mwanamke huyo alijiuliza maswali gani?

      • Kujifunza Biblia kulimsaidiaje?

      Biblia inatutia moyo tuulize maswali. Soma Mathayo 7:7, kisha mzungumzie swali hili:

      • Wewe hujiuliza maswali gani ambayo yanaweza kujibiwa na Biblia?

      5. Unaweza kufurahia kusoma Biblia

      Watu wengi wanafurahia kusoma Biblia na wananufaika kwa kufanya hivyo. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali haya:

      VIDEO: Kusoma Biblia (2:05)

      • Katika video hiyo, vijana hao walihisije kuhusu kusoma?

      • Kwa nini sasa wanapenda kusoma Biblia?

      Biblia inasema kwamba inaweza kutupatia mwongozo unaotupatia faraja na tumaini. Soma Waroma 15:4, kisha mzungumzie swali hili:

      • Je, unafurahia ahadi ya Biblia ya kukupatia faraja na tumaini?

      6. Watu wengine wanaweza kutusaidia kuelewa Biblia

      Zaidi ya kusoma Biblia wakiwa peke yao, watu wengi wametambua kwamba wanaielewa vizuri zaidi wanaposaidiwa na watu wengine. Soma Matendo 8:26-31, kisha mzungumzie swali hili:

      • Tunawezaje kuielewa Biblia vizuri?​—Ona mstari wa 30 na 31.

      Picha: 1. Mweneza-injili Filipo anamfafanulia Maandiko mwanamume Mwethiopia. 2. Shahidi wa Yehova akijifunza Biblia pamoja na mama na watoto wake wawili.

      Mwanamume Mwethiopia alihitaji msaada ili kuelewa Maandiko. Leo watu wengi wananufaika kwa kujifunza Biblia pamoja na wengine

      WATU FULANI HUSEMA: “Kujifunza Biblia ni kupoteza wakati.”

      • Wewe una maoni gani? Kwa nini?

      MUHTASARI

      Biblia inatoa ushauri mzuri kuhusu maisha ya kila siku, inajibu maswali muhimu, na inawapa watu faraja na tumaini.

      Ungejibuje?

      • Biblia inatoa ushauri wa aina gani?

      • Biblia inajibu maswali gani?

      • Ungependa kujifunza nini katika Biblia?

      Lengo

      CHUNGUZA ZAIDI

      Jifunze jinsi ushauri wa Biblia unavyotufaa leo.

      “Mafundisho ya Biblia​—Hekima Isiyopitwa na Wakati” (Mnara wa Mlinzi Na. 1 2018)

      Ona jinsi Biblia ilivyomsaidia mwanamume aliyepambana na hisia mbaya tangu utotoni.

      Jinsi Nilivyoanza Kufurahia Maisha Mapya (2:53)

      Chunguza ushauri wa Biblia kuhusu maisha ya familia.

      “Siri 12 za Mafanikio Katika Familia” (Amkeni! Na. 2 2018)

      Jifunze jinsi Biblia inavyofunua ukweli kuhusu yule anayeutawala ulimwengu huu.

      Kwa Nini Ujifunze Biblia?​—Video Nzima (3:14)

  • Biblia Ni Ujumbe Kutoka kwa Mungu
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 1. Ikiwa Biblia iliandikwa na wanadamu, kwa nini tunasema ni Neno la Mungu?

      Biblia iliandikwa na watu 40 kwa kipindi cha miaka 1,600 hivi, kuanzia mwaka wa 1513 K.W.K. hadi 98 W.K. Waandikaji hao walitoka katika malezi mbalimbali. Ingawa hivyo, ujumbe walioandika unapatana. Linawezekanaje? Hilo linawezekana kwa sababu Mungu ndiye Mtungaji wa Biblia. (Soma 1 Wathesalonike 2:13.) Waandikaji hao hawakuandika mawazo yao wenyewe. Badala yake, “walisema yaliyotoka kwa Mungu kama walivyoongozwa na roho takatifu.”a (2 Petro 1:21) Mungu alitumia roho yake takatifu kuwaongoza au kuwachochea watu hao waandike mawazo yake.​—2 Timotheo 3:16.

  • Biblia Ni Ujumbe Kutoka kwa Mungu
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 4. Biblia inatuambia ni nani aliyeitunga

      Onyesha VIDEO. Kisha soma 2 Timotheo 3:16, na mzungumzie maswali yanayofuata.

      VIDEO: Ni Nani Aliyeitunga Biblia?​—Kisehemu (2:48)

      • Ikiwa Biblia iliandikwa na wanadamu, kwa nini inaitwa Neno la Mungu?

      • Je, unafikiri inapatana na akili kuamini kwamba Mungu aliwatumia wanadamu kuwasilisha mawazo yake?

      Bosi akimpa karani ujumbe, naye karani anaandika mawazo hayo kwenye barua.

      Karani anaweza kuandika barua yenye ujumbe kutoka kwa bosi wake. Vivyo hivyo, wanadamu waliandika Biblia, lakini ujumbe wake ulitoka kwa Mungu

  • Biblia Ni Ujumbe Kutoka kwa Mungu
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki