Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kitabu cha Biblia Namba 55—2 Timotheo
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 7. Kwa nini Maandiko yaliyopuliziwa na Mungu yapasa kuwa yenye mafaa hasa katika “siku za mwisho”?

      7 “Katika siku za mwisho,” kutakuwako nyakati zilizo ngumu kushughulika nazo na watu wanaothibitika kuwa bandia kwa onyesho lao la ujitoaji kimungu, “sikuzote wakijifunza na bado wasiweze kamwe kufikia maarifa sahihi ya ukweli.” Lakini Timotheo amefuata kwa ukaribu fundisho la Paulo, mwendo wake wa maisha, na minyanyaso yake, ambayo Bwana alimkomboa kutoka kwayo. “Kwa uhakika,” yeye aongezea, “wote wale wanaotamani kuishi kwa ujitoaji kimungu katika ushirika pamoja na Kristo Yesu watanyanyaswa pia.” (NW) Hata hivyo, Timotheo apaswa aendelee katika mambo aliyojifunza kuanzia utoto mchanga, ambayo yaweza kumhekimisha kwa ajili ya wokovu, kwa maana “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa.”—3:1, 7, 12, 16.

  • Kitabu cha Biblia Namba 55—2 Timotheo
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 10. (a) Ni mafaa gani hasa ya “kila andiko” inayokaziwa katika Timotheo wa Pili, nao Wakristo wapaswa kujitahidi kuwa nini? (b) Ni uvutano gani upaswao kuepukwa, nalo hilo laweza kufanywaje? (c) Kwaendelea kuwa uhitaji wenye uharaka kwa ajili ya nini?

      10 “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa.” Lina mafaa kwa ajili ya nini? Paulo atuambia hivi katika barua yake ya pili kwa Timotheo: “Kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.” (3:16, 17) Kwa hiyo mafaa ya “mafundisho” yakaziwa katika barua hii. Wapenda uadilifu wote leo watataka kufuata shauri lenye hekima la barua hiyo kwa kujitahidi kuwa walimu wa Neno na katika kufanya yote yote ili kuwa wafanya kazi wa Mungu waliokubaliwa, ‘wakitumia kwa halali neno la kweli.’ Kama katika Efeso ya siku za Timotheo, ndivyo katika kizazi cha ki-siku-hizi, kuna wale wanaojishughulisha katika “maswali ya upumbavu yasiyo na elimu,” ambao “wakijifunza sikuzote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli,” na wanaokataa “mafundisho yenye uzima” kwa kupendelea walimu wanaotekenya masikio yao jinsi wanavyotaka kwa ubinafsi. (2:15, 23; 3:7; 4:3, 4) Ili kuepuka uvutano huo wa kilimwengu wenye kuchafua, ni lazima kuendelea ‘kushika kielelezo cha maneno yenye uzima’ katika imani na upendo. Zaidi ya hayo, kuna uhitaji wenye uharaka wa watu zaidi na zaidi ‘kufaa kufundisha wengine’ ndani na nje ya kundi pia, kama vile Timotheo, “mtumwa wa Bwana.” Wenye furaha ni wote wanaobeba daraka hilo, kuwa ‘wanaofaa kufundisha kwa uanana,’ na wanaohubiri neno “kwa uvumilivu wote na mafundisho”!—1:13; 2:2, 24, 25; 4:2.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki