Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Marko ‘Mwenye Faida kwa Ajili ya Huduma’
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
    • Paulo alipofungwa gerezani kwa mara ya pili huko Roma karibu mwaka wa 65 W.K., alimwandikia Timotheo huko Efeso na kuongezea hivi: “Umchukue Marko na uje pamoja naye.” (2 Tim. 4:11) Kwa hiyo, wakati huo Marko alikuwa Efeso. Hatuna shaka yoyote kwamba alikubali ombi la Paulo la kurudi Roma pamoja na Timotheo. Safari zilikuwa ngumu wakati huo, lakini Marko alifunga safari hizo kwa kupenda.

  • Marko ‘Mwenye Faida kwa Ajili ya Huduma’
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
    • “Mwenye Faida Kwangu kwa Ajili ya Huduma”

      Zaidi ya kuandika Injili yake, Marko alifanya mambo mengine huko Roma. Kumbuka maneno ambayo Paulo alimwambia Timotheo: “Umchukue Marko na uje pamoja naye.” Kwa nini Paulo alisema hivyo? “Kwa maana yeye ni mwenye faida kwangu kwa ajili ya huduma.”—2 Tim. 4:11.

      Uhakika wa kwamba Marko anatajwa katika vitabu vya Maandiko vilivyoandikwa mwisho unafunua mengi kumhusu. Katika masimulizi yote kuhusu utendaji wake kutanikoni, Marko hatajwi popote kuwa mtume, kiongozi, au nabii. Alikuwa mhudumu, yaani, aliwahudumia na kuwatumikia wengine. Na muda mfupi kabla ya kifo cha Paulo, bila shaka Marko alimsaidia sana mtume huyo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki