Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mtegemee Yehova Sikuzote!
    Mnara wa Mlinzi—2015 | Aprili 15
    • 2 Inawezekana kwamba mtume Paulo alifungwa huko Roma kwa mara ya pili kulipokuwa na hali hizo ngumu. Je, Wakristo wengine wangekuja kumsaidia? Huenda mwanzoni Paulo alihangaishwa na jambo hilo, kwani alimwandikia hivi Timotheo: “Katika kujitetea kwangu mara ya kwanza hakuna yeyote aliyekuja upande wangu, bali wote waliniacha—hilo lisihesabiwe kwao.” Hata hivyo, Paulo alitambua kwamba hakuwa peke yake. Aliandika hivi: “Lakini Bwana alisimama karibu nami na kutia nguvu ndani yangu.” Naam, Bwana Yesu alimpa Paulo nguvu alizohitaji. Msaada huo ulikuwa na matokeo gani kwa Paulo? Alisema hivi: “Nilikombolewa kutoka katika kinywa cha simba.”—2 Tim. 4:16, 17.a

      3 Paulo alikumbuka jinsi Yehova alivyomsaidia awali, na hilo lilimwimarisha, na kumsaidia awe na imani kwamba Yehova atamtegemeza ili avumilie majaribu aliyokuwa akikabili, na hali ngumu yoyote ambayo huenda ingejitokeza baadaye. Kwa kweli, hiyo ndiyo sababu alisema hivi: “Bwana atanikomboa kutoka katika kila tendo la uovu.” (2 Tim. 4:18) Naam, Paulo alijifunza kwamba hata kama wanadamu hawangemsaidia, kwa hakika Yehova na Yesu wangemsaidia!

  • Mtegemee Yehova Sikuzote!
    Mnara wa Mlinzi—2015 | Aprili 15
    • “KINYWA CHA SIMBA”

      10-12. (a) Ni hali gani zinaweza kufanya mambo yawe magumu wakati wa kumuuguza mtu wa familia? (b) Uhusiano wako na Yehova unaathiriwaje unapomtegemea ukiwa katika hali ngumu? Toa mfano.

      10 Unapokabili hali ngumu sana, huenda ukahisi kama mtume Paulo alivyohisi, yaani, uko katika au unakaribia kuwa katika “kinywa cha simba.” Ni muhimu sana kumtegemea Yehova nyakati kama hizo, ingawa si rahisi kufanya hivyo. Kwa mfano, wazia unamuuguza mtu wa familia anayeumwa ugonjwa usio na tiba. Labda umemwomba Yehova akupe hekima na nguvu.b Kwa kuwa umefanya yote unayoweza, je, huhisi umepata amani kwa kujua kwamba Yehova anaona na atakupa msaada unaohitaji ili ubaki mwaminifu na uendelee kuvumilia?—Zab. 32:8.

  • Mtegemee Yehova Sikuzote!
    Mnara wa Mlinzi—2015 | Aprili 15
    • a “Kinywa cha simba” ambacho Paulo alikombolewa huenda kilimaanisha kinywa cha simba halisi au ulikuwa mfano tu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki