-
Akina Mama—Jifunzeni Kutokana na Mfano wa EunikeMnara wa Mlinzi (Funzo)—2022 | Aprili
-
-
WAFUNDISHE WATOTO WAKO KUPITIA MAMBO UNAYOFANYA
12. Kulingana na 2 Timotheo 1:5, mfano wa Eunike ulikuwa na matokeo gani kwa Timotheo?
12 Soma 2 Timotheo 1:5. Eunike alimwekea mfano mzuri Timotheo. Ni lazima alimfundisha kwamba imani ya kweli inahusisha matendo. (Yak. 2:26) Bila shaka, Timotheo aliona kwamba matendo ya mama yake yalichochewa na upendo wake wenye nguvu kwa Yehova. Kwa kweli, Timotheo alijionea kwamba kumtumikia Yehova kulimfanya mama yake awe na furaha. Mfano wa Eunike ulikuwa na matokeo gani kwa Timotheo? Kama mtume Paulo alivyotaja, Timotheo alikuwa na imani yenye nguvu kama ya mama yake. Hilo halikujitokeza lenyewe. Timotheo alikuwa ameona mfano wa mama yake, naye alichochewa kumwiga. Vivyo hivyo leo, akina mama wengi wamegusa mioyo ya watu wa familia zao “bila neno.” (1 Pet. 3:1, 2) Unaweza kufanya vivyo hivyo pia. Jinsi gani?
13. Kwa nini mama anapaswa kutanguliza maishani uhusiano wake pamoja na Yehova?
13 Tanguliza maishani uhusiano wako na Yehova. (Kum. 6:5, 6) Kama ilivyo kwa mama wengi, unajidhabihu kwa njia nyingi. Unadhabihu muda, pesa, usingizi, na mambo mengine ili kuwaandalia watoto wako mahitaji yao ya kimwili. Lakini hupaswi kamwe kutumia muda mwingi sana kufanya mambo hayo, hivi kwamba unakosa muda wa kuimarisha uhusiano wako pamoja na Yehova. Tenga kwa ukawaida muda kwa ajili ya kusali kibinafsi, kujifunza Biblia kibinafsi, na kuhudhuria mikutano ya kutaniko. Kwa kufanya hivyo, utajiimarisha kiroho na kuiwekea mfano mzuri familia yako na pia watu wengine.
-
-
Akina Mama—Jifunzeni Kutokana na Mfano wa EunikeMnara wa Mlinzi (Funzo)—2022 | Aprili
-
-
16. Mfano wa akina mama unaweza kuwachocheaje wengine?
16 Akina mama, kumbukeni kwamba mfano wenu unaweza kuwachochea wengine. Jinsi gani? Fikiria jinsi mfano wa Eunike ulivyomchochea mtume Paulo. Alitambua kwamba imani ya Timotheo isiyo na unafiki, “kwanza ilikuwa ndani ya . . . Eunike.” (2 Tim. 1:5) Paulo aliona imani ya Eunike kwa mara ya kwanza lini? Inaelekea ilikuwa wakati wa safari yake ya kwanza ya umishonari alipokutana na Loisi na Eunike huko Listra, na huenda aliwasaidia kuwa Wakristo. (Mdo. 14:4-18) Hebu wazia: Paulo alipomwandikia Timotheo—miaka 15 hivi baadaye—bado alikumbuka matendo ya uaminifu ya Eunike naye alimtaja kuwa mfano unaostahili kuigwa! Ni wazi kwamba mfano wake ulimtia moyo sana mtume Paulo na inaelekea pia Wakristo wengine wengi wa karne ya kwanza. Ikiwa unawalea watoto wako bila mwenzi au uko katika familia iliyogawanyika kidini, uwe na uhakika kwamba mfano wako wa uaminifu utawaimarisha na kuwachochea wale wanaokuzunguka.
-