-
Ni Nini Kitakachokusaidia Uendelee Kujifunza Biblia?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
5. Endelea kujifunza licha ya upinzani
Wakati mwingine, huenda watu wakajaribu kukuvunja moyo uache kujifunza Biblia. Ona mfano wa Francesco. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.
Katika video hiyo, familia na marafiki wa Francesco walitendaje alipowaambia mambo aliyokuwa akijifunza?
Alinufaikaje kwa kuendelea kujifunza Biblia?
Soma 2 Timotheo 2:24, 25, kisha mzungumzie maswali haya:
Marafiki na watu wa familia yako wanahisije kuhusu mambo unayojifunza?
Kulingana na mistari hii, unapaswa kufanya nini ikiwa mtu fulani hafurahii kukuona ukijifunza Biblia? Kwa nini?
-
-
Unawezaje Kuwahubiria Wengine Habari Njema?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
Unapowaambia wengine kuhusu habari njema, fikiria jambo utakalosema na jinsi utakavyolisema. Soma 2 Timotheo 2:24 na 1 Petro 3:15, kisha mzungumzie maswali haya:
Unaweza kutumiaje ushauri ulio katika maandiko haya unapozungumza na wengine kuhusu Biblia?
Huenda baadhi ya watu wa familia yako na marafiki wasikubaliane na mambo unayowaambia. Unaweza kufanya nini? Utaepuka kufanya nini?
Kwa nini ni vizuri kutumia maswali kwa busara badala ya kuwalazimisha waamini mambo unayosema?
-