Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Waangalizi Wanaochunga Kundi
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • 11 Wanaume wanaostahili kuwa waangalizi wanaonyesha kiasi katika mazoea na wanaposhughulika na wengine. Hawapaswi kuwa washupavu. Badala yake, wanapaswa kuwa na usawaziko na wanaojidhibiti. Wanapaswa kuwa na kiasi katika kula, kunywa, tafrija, mambo wanayopenda, na burudani. Wanakunywa pombe kwa kiasi ili wasishtakiwe kwa madai ya ulevi au wasiwe na shtaka la kuwa walevi. Mtu ambaye hisi zake zimepumbazwa na pombe hushindwa kujidhibiti, naye hawezi kushughulikia mahitaji ya kiroho ya kutaniko.

  • Waangalizi Wanaochunga Kundi
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • 13 Mwangalizi anapaswa kuwa na usawaziko. Anapaswa kuwa na uwezo wa kufanya kazi kwa umoja na kushirikiana na wengine katika baraza la wazee. Anapaswa kuwa na maoni yanayofaa kujihusu na hapaswi kudai mengi kutoka kwa wengine. Mwangalizi mwenye usawaziko hashikilii sana maoni yake, wala haoni maoni yake kuwa bora kuliko ya wazee wenzake. Wengine wanaweza kuwa na sifa au uwezo fulani ambao yeye hana. Usawaziko wake hutokana na kufanya maamuzi yanayotegemea Maandiko na kujitahidi kumwiga Yesu Kristo. (Flp. 2:2-8) Mzee si mgomvi au mkatili, bali anawaheshimu wengine, akiwaona kuwa bora kuliko yeye. Si mshupavu, akisisitiza kila mara kwamba njia yake au maoni yake yanapaswa kukubalika. Hapaswi kuwa mwenye kukasirika upesi, bali anapaswa kushughulika na wengine kwa amani.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki