-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—2001 | Oktoba 1
-
-
Mtume Paulo aliwaandikia hivi Wakristo Waebrania wa karne ya kwanza: “Kumebaki pumziko la sabato kwa watu wa Mungu. Kwa maana mtu ambaye ameingia ndani ya pumziko la Mungu amepumzika pia mwenyewe kutokana na kazi zake mwenyewe, kama vile Mungu alivyofanya kutokana na zake mwenyewe. Kwa hiyo acheni sisi tufanye yote kabisa tuwezayo ili kuingia ndani ya pumziko hilo.”—Waebrania 4:9-11.
-
-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—2001 | Oktoba 1
-
-
Tukirejezea maneno ya Paulo kwa Waebrania, twaona alitaja kwamba “kumebaki pumziko la sabato kwa watu wa Mungu,” hivyo akawahimiza Wakristo wenzake wafanye yote wawezayo “ili kuingia ndani ya pumziko hilo.” Hilo laonyesha kwamba Paulo alipoandika maneno hayo, “siku ya saba” ya pumziko la Mungu, iliyokuwa imeanza miaka 4,000 hivi mapema, ilikuwa bado inaendelea. Siku hiyo haitaisha hadi kusudi la Mungu kwa wanadamu na dunia litimizwe kabisa mwishoni mwa Utawala wa Miaka Elfu wa Yesu Kristo, ambaye ni “Bwana wa sabato.”—Mathayo 12:8; Ufunuo 20:1-6; 21:1-4.
-
-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—2001 | Oktoba 1
-
-
Bila shaka, mazungumzo ya Paulo kuhusu pumziko la Mungu na jinsi mtu awezavyo kuingia katika pumziko hilo, yaliwatia moyo Wakristo Waebrania huko Yerusalemu, ambao walikuwa wamevumilia mnyanyaso na dhihaka nyingi kwa sababu ya imani yao. (Matendo 8:1; 12:1-5) Vivyo hivyo, maneno ya Paulo yanaweza kuwatia moyo Wakristo leo. Sisi pia tunapaswa kupumzika kutokana na kazi zetu wenyewe na kufanya yote tuwezayo kuingia ndani ya pumziko hilo. Tunafanya hivyo kwa kuwa tunatambua kwamba kutimizwa kwa ahadi ya Mungu ya kuleta dunia paradiso chini ya Ufalme wake wenye uadilifu kumekaribia sana.—Mathayo 6:10, 33; 2 Petro 3:13.
-