Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Umeingia Katika Pumziko la Mungu?
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 15
    • “Neno la Mungu Liko Hai”

      20. Tunaweza kuelewa andiko la Waebrania 4:12 katika njia gani mbili? (Ona maelezo ya chini.)

      20 Paulo alipoandika kwamba “neno la Mungu liko hai,” hakuwa akizungumzia hasa Neno la Mungu lililoandikwa, yaani, Biblia.c Mistari mingine katika sura hiyo inaonyesha kwamba alikuwa akizungumza kuhusu ahadi za Mungu. Paulo alikuwa akisema kwamba sikuzote Mungu anatimiza ahadi zake. Yehova alionyesha ukweli wa jambo hilo kupitia nabii Isaya kwa kusema: “Neno langu . . . halitarudi kwangu bila matokeo, bali . . . litafanikiwa katika yale ambayo nimelituma.” (Isa. 55:11) Hivyo, tunahitaji kuwa wenye subira ikiwa mambo hayafanyiki haraka kama tunavyotazamia. Tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova ‘anaendelea kufanya kazi’ ili kutimiza kabisa kwa mafanikio kusudi lake.—Yoh. 5:17.

      21. Andiko la Waebrania 4:12 linaweza jinsi gani kuwatia moyo washiriki waaminifu waliozeeka wa “umati mkubwa”?

      21 Washiriki waaminifu waliozeeka wa “umati mkubwa” wamemtumikia Yehova kwa makumi ya miaka. (Ufu. 7:9) Wengi wao hawakutazamia kwamba wangezeeka katika mfumo huu wa mambo. Hata hivyo, hawavunjiki moyo. (Zab. 92:14) Wanajua kwamba ahadi za Mungu ni za kweli, ziko hai, na Yehova anafanya kazi ili kuzitimiza. Kwa kuwa Mungu anathamini kutoka moyoni kusudi lake, tunamfanya ashangilie tunapoonyesha kwamba kusudi hilo ni la maana kwetu pia. Katika siku hii ya saba ya pumziko, hakuna jambo ambalo litamzuia Yehova kukamilisha kusudi lake. Na anajua kwamba watu wake, wakiwa kikundi, wataendelea kutenda kupatana na kusudi lake. Namna gani wewe? Je, wewe binafsi umeingia katika pumziko la Mungu?

  • Je, Umeingia Katika Pumziko la Mungu?
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 15
    • c Leo, Mungu anazungumza nasi kupitia Neno lake lililoandikwa, Biblia, ambalo lina nguvu ya kubadili maisha yetu. Kwa hiyo, yale tunayosoma katika Waebrania 4:12 ni kweli pia kuhusu Biblia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki