Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mikutano ya Mashahidi wa Yehova Inaweza Kukunufaishaje?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • Somo la 10. Mwanamume akiangalia andiko analoonyeshwa kwenye Biblia wakati wa mkutano wa Mashahidi wa Yehova.

      SOMO LA 10

      Mikutano ya Mashahidi wa Yehova Inaweza Kukunufaishaje?

      Je, umewahi kualikwa uhudhurie mkutano wa Mashahidi wa Yehova? Ikiwa hujawahi kuhudhuria, huenda ukawa na wasiwasi unapoalikwa uhudhurie kwa mara ya kwanza. Huenda ukajiuliza: ‘Ni nini hufanyika katika mikutano hiyo? Kwa nini mikutano hiyo ni muhimu? Kwa nini ninapaswa kuhudhuria?’ Katika somo hili utajifunza jinsi mikutano hiyo inavyoweza kukunufaisha na kukusaidia uwe na uhusiano wa karibu zaidi na Mungu.

      1. Kwa nini ni muhimu sana kukutana pamoja?

      Mwandikaji fulani wa Biblia alitaja sababu muhimu zaidi ya kukutana pamoja, alisema: “Katika kutaniko kubwa, nitamsifu Yehova.” (Zaburi 26:12) Vivyo hivyo, Mashahidi wa Yehova hufurahia sana kukutana pamoja. Ulimwenguni pote, wao hukutana kila juma ili kumsifu Mungu, kuimba, na kusali. Kila mwaka, wao pia hukutana mara chache katika vikundi vikubwa zaidi ili kumwabudu Mungu.

      2. Utajifunza nini katika mikutano yetu?

      Katika mikutano, sisi hujifunza Neno la Mungu, “[tunalifafanua] waziwazi na kueleza maana yake.” (Soma Nehemia 8:8.) Ukihudhuria mikutano, utajifunza kumhusu Yehova na sifa zake zenye kupendeza. Unapojifunza mengi kuhusu jinsi anavyokupenda, ndivyo utakavyozidi kuwa na uhusiano wa karibu naye. Vilevile utajifunza jinsi anavyoweza kukusaidia uwe na maisha yenye kuridhisha.​—Isaya 48:17, 18.

      3. Utanufaikaje kwa kushirikiana na wengine katika mikutano?

      Yehova anatuagiza “tufikiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri, bila kuacha kukutana pamoja.” (Waebrania 10:24, 25) Katika mikutano yetu, utakutana na watu wanaopendana sana na ambao, kama wewe, wanataka kujifunza mengi kumhusu Mungu. Utawasikia wakizungumza kuhusu mambo yenye kutia moyo kutoka kwenye Biblia. (Soma Waroma 1:11, 12.) Vilevile utawafahamu wengine ambao wamefaulu kukabiliana na matatizo yanayowapata watu waliofunga ndoa au ambao hawajafunga ndoa. Hizo ni baadhi ya sababu chache zinazofanya tutii agizo la Yehova la kukutana pamoja kwa ukawaida!

      CHIMBA ZAIDI

      Jifunze mambo yanayotendeka katika mikutano ya Mashahidi wa Yehova na kwa nini ni muhimu tujitahidi kuhudhuria mikutano hiyo.

      4. Mikutano ya Mashahidi wa Yehova

      Katika karne ya kwanza, Wakristo walikutana kwa ukawaida ili kumwabudu Yehova. (Waroma 16:3-5) Soma Wakolosai 3:16, kisha mzungumzie swali hili:

      • Wakristo wa karne ya kwanza walimwabudu Yehova jinsi gani?

      Leo, Mashahidi wa Yehova hukutana kwa ukawaida katika maeneo yao ya ibada. Ili kuona mambo yanayotendeka katika mikutano, onyesha VIDEO. Kisha, mtazame picha ya mikutano ya kutaniko iliyo kwenye ukurasa huu na mzungumzie maswali haya:

      VIDEO: Ni Nini Hutendeka Katika Jumba la Ufalme? (2:12)

      • Uliona mambo gani katika Jumba la Ufalme ambayo yametajwa kwenye Wakolosai 3:16?

      • Ni jambo gani lingine lililokupendeza kwenye video au picha kuhusu mikutano?

      Soma 2 Wakorintho 9:7, kisha mzungumzie swali hili:

      • Kwa nini hakuna malipo ya kiingilio kwenye mikutano ya Mashahidi wa Yehova?

      Chunguza pamoja na mwalimu wako mambo ambayo yatazungumziwa kwenye mkutano juma hili.

      • Unafikiri utafurahia au kunufaika zaidi na sehemu gani ya mkutano?

      Je, wajua?

      Kwenye jw.org, unaweza kupata mahali na wakati ambao mikutano hufanywa ulimwenguni pote.

      Picha: Mambo yanayoendelea kwenye Jumba la Ufalme kabla ya mkutano, wakati wa mkutano, na baada ya mkutano. Mambo hayo yanaonekana kwenye picha ya A hadi D. A. Shahidi wa Yehova akitoa hotuba inayotegemea Biblia kwenye mkutano. B. Dada Shahidi aliyehudhuria mkutano akitoa maelezo. C. Shahidi wa Yehova akizungumza na familia baada ya mkutano. D. Shahidi wa Yehova akimfungulia mlango mtu aliyezeeka anayefika kwenye mkutano.
      1. Mikutano yetu inatia ndani hotuba, maigizo, na video. Mikutano huanza na kumalizika kwa wimbo na sala

      2. Katika baadhi ya sehemu za mkutano wasikilizaji hukaribishwa kutoa maelezo

      3. Watu wote wanakaribishwa​—watu wenye familia, waseja, waliozeeka, na watoto

      4. Hakuna malipo ya kiingilio wala sadaka zinazokusanywa kwenye mikutano ya Mashahidi wa Yehova

      5. Jitihada inahitajika ili kuhudhuria mikutano

      Fikiria hali ilivyokuwa katika familia ya Yesu. Kila mwaka, walitembea kwa siku kadhaa umbali wa kilomita 100 hivi kwenye eneo lenye milima kutoka Nazareti hadi Yerusalemu ili kwenda hekaluni. Soma Luka 2:39-42, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Je, unafikiri safari hiyo ya kwenda Yerusalemu ilihitaji jitihada zozote?

      • Kwa nini huenda ukahitaji kujitahidi ili uhudhurie mikutano?

      • Je, unafikiri jitihada hizo ni muhimu? Kwa nini?

      Picha: Yosefu, Maria, na ndugu za Yesu wakijiandaa kwa ajili ya safari. 1. Yosefu akipakia mizigo juu ya punda, na Maria akitayarisha vyakula. 2. Ramani inayoonyesha safari ya kutoka Nazareti kwenda Yerusalemu.

      Biblia inasema kwamba ni muhimu sana kukutana pamoja ili kuabudu. Soma Waebrania 10:24, 25, kisha mzungumzie swali hili:

      • Kwa nini tunapaswa kuhudhuria mikutano kwa ukawaida?

      WATU FULANI HUSEMA: “Si lazima ukusanyike pamoja na watu wengine. Inatosha kusoma Biblia ukiwa nyumbani.”

      • Ni andiko au mfano gani ulio katika Biblia unaoonyesha jambo ambalo Yehova anataka tufanye?

      MUHTASARI

      Kuhudhuria mikutano kutakusaidia ujifunze mengi kumhusu Yehova, uimarishe urafiki wako pamoja naye, na umwabudu ukiwa pamoja na watu wengine.

      Ungejibuje?

      • Kwa nini Yehova anatutia moyo tukutane pamoja?

      • Utajifunza mambo gani kwenye mikutano ya Mashahidi wa Yehova?

      • Unafikiri utanufaika kwa njia gani nyingine ukihudhuria mikutano?

      Lengo

      CHUNGUZA ZAIDI

      Vipi ikiwa una wasiwasi kuhusu kuhudhuria mkutano? Ona jambo lililomsaidia mwanamume aliyehisi hivyo apende mikutano.

      Hatutasahau Tulivyokaribishwa (4:17)

      Ona jinsi kijana fulani alivyofurahia mikutano na jambo alilofanya ili kuendelea kuhudhuria.

      Nilifurahia Sana Mikutano! (4:33)

      Jifunze jinsi wengine wanavyohisi kuhusu kuhudhuria mikutano.

      “Kwa Nini Uhudhurie Mikutano Kwenye Jumba la Ufalme?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

      Ona jinsi maisha ya mwanamume aliyeshirikiana na wahalifu yalivyobadilika alipohudhuria mkutano wa Mashahidi wa Yehova.

      “Nilitembea na Bunduki Kila Wakati” (Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 2014)

  • Ufalme wa Mungu Umeanza Kutawala!
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 5. Ulimwengu umebadilika tangu mwaka wa 1914

      Onyesha VIDEO.

      VIDEO: Ulimwengu Umebadilika Tangu Mwaka wa 1914 (1:10)

      Yesu alitabiri kuhusu hali ambazo zingekuwa ulimwenguni wakati ambapo angeanza kutawala. Soma Luka 21:9-11, kisha mzungumzie swali hili:

      • Umesikia au kujionea nini kati ya mambo hayo yaliyotabiriwa?

      Mtume Paulo alifafanua jinsi ambavyo watu wangetenda wakati wa siku za mwisho za utawala wa wanadamu. Soma 2 Timotheo 3:1-5, kisha mzungumzie swali hili:

      • Umejionea watu wakiwa na tabia gani kati ya tabia hizo?

      Picha: Picha zinazoonyesha hali za ulimwengu na tabia za watu katika siku za mwisho. 1. Kiongozi wa jeshi akihutubu jukwaani kwa sauti kubwa akiwa ameinua mikono. 2. Majengo yaliyobomoka baada ya tetemeko la ardhi. 3. Ndege za vita. 4. Watu waliovaa barakoa wakitembea. 5. Majengo mawili jijini New York yanawaka moto baada ya shambulizi la kigaidi. 6. Mwanamume akitumia dawa za kulevya. 7. Mume akiwa amekunja ngumi akimgombeza mke wake. 8. Pombe na dawa mbalimbali za kulevya. 9. Wanawake wawili waliovaa mavazi ya kisasa na mapambo ya thamani wakijipiga picha. 10. Mtumbuizaji anatumbuiza umati wa watu. 11. Mwandamanaji akirusha bomu la petroli.

      6. Utawala wa Ufalme wa Mungu unapaswa kutuchochea kutenda

      Soma Mathayo 24:3, 14, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Ni kazi gani muhimu inayoonyesha kwamba Ufalme wa Mungu unatawala?

      • Unawezaje kushiriki kufanya kazi hiyo?

      Sasa Ufalme wa Mungu unatawala, na hivi karibuni utaitawala dunia yote. Soma Waebrania 10:24, 25, kisha mzungumzie swali hili:

      • Kila mmoja wetu anapaswa kufanya nini ‘kadiri tunavyoona siku ile ikikaribia’?

      Picha: 1. Mwanafunzi wa Biblia akiwa amehudhuria mkutano wa Mashahidi wa Yehova. 2. Mwanafunzi huyo wa Biblia anamhubiria mtu anayemfahamu.

      Unapojifunza jambo linaloweza kuwasaidia au kuwaokoa wengine, unapaswa kufanya nini?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki