Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/90 uku. 3
  • Desturi Yako Ni Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Desturi Yako Ni Nini?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • TIANENI MOYO
  • Mikutano ya Mashahidi wa Yehova Inaweza Kukunufaishaje?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Kwa Nini Tunapaswa Kukutanika Pamoja kwa Ajili ya Ibada?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Kuthamini Makusanyiko ya Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Jinsi ya Kupata Shangwe Zaidi Kutokana na Mikutano
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 5/90 uku. 3

Desturi Yako Ni Nini?

1 Mikutano ya Kikristo ni sehemu ya muhimu ya ibada yetu kwa Yehova. Mtume Paulo kwa kufaa atusihi tusiache kukusanyika pamoja, “kama ilivyo desturi ya wengine.”—Ebr. 10:25.

2 Je! wewe una hisia izo hizo kuhusu kushirikiana na ndugu zako kwenye mikutano ya Kikristo? Desturi yako yafunua nini katika hilo? Je! wewe wahudhuria kwa ukawaida mikutano yote, kutia ndani Funzo la Kitabu la Kundi? Au je! waona kwamba kwa desturi unakosa mikutano? Mikutano ina mahali gani maishani mwako? Je! wewe unatia moyo wengine wahudhurie mikutano kwa ukawaida? Je! wewe umekuwa ukitia moyo wahudhuriaji Ukumbusho wawe wa kawaida katika uhudhuriaji wao wa mikutano?

3 Hata kawaida yetu ya kila siku iwe nini, ushauri wa Paulo hauwezi kupunguzwa uzito. Ingawa yaeleweka kwamba pindi kwa pindi Mkristo aweza kulazimika kukosa mkutano mmoja kwa sababu ya afya mbaya au mambo mengine asiyoweza kudhibiti, hakika haipasi kuwa desturi yake. (Rum. 2:21) Kukiwako wajibu mwingi wa kushughulikia, ambao huenda ukatia ndani baadhi ya utendaji wa kitheokrasi, Mkristo ahitaji kuhakikisha mambo yaliyo ya maana zaidi. (Flp. 1:10) Mikutano yatiwa miongoni mwa mambo ya maana zaidi kwa Mkristo na ni ya muhimu kwa ajili ya hali yetu njema.

TIANENI MOYO

4 Paulo alipowaandikia Waroma, alisema kwamba alikuwa anatamani kuwaona. Kwa nini? Kusudi atoe zawadi fulani ya kiroho ili kwamba ‘wafanywe imara.’ (Rum. 1:11) Yeye hakuridhika tu na kuwatumia barua, habari iliyoandikwa ili wasome, bali alihisi kwamba ushirikiano ulikuwa wa maana, ndiyo, ulihitajiwa, kwa kuwa aliendelea kusema: “Tufarijiane [Ili kuwe badilishano la kitia-moyo, NW].” Au kama ambavyo kielezi-chini katika Reference Bible kinavyotaarifu: “Tutiwe moyo pamoja.” (Rum. 1:12) Hata Paulo, mtume, alitambua uhitaji wake wa kitia-moyo kupitia ushirika wa Kikristo.

5 Vivyo hivyo, kwenye mikutano yetu twapaswa kuchocheana kwenye upendo na kazi njema. Tabasamu ya kirafiki na salamu ya uchangamfu vyaweza kuwa na tokeo chanya juu ya wengine. Maelezo yenye kujenga, sehemu zilizotayarishwa vizuri kwenye programu, kuona wengine wakifanya maendeleo ya kiroho, na kule kuwa tu miongoni mwa ndugu penye mikutano kwaweza kutia moyo sana. Hata kama tumechoka mwishoni mwa siku, kwa kawaida tutakuta kwamba twahisi vizuri zaidi baada ya kuhudhuria mkutano. Urafiki wa Kikristo na upendo ambao ndugu zetu wanatuonyesha vitatutia moyo “Tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu.” (Ebr. 12:1) Kwa kusikiliza kwa uangalifu Neno la Mungu, twaweza kutayarishwa kushikilia kwa imara tangazo rasmi la peupe la tumaini letu bila kutikisika. Kweli kweli, kuna baraka nyingi zinazoletwa na kuwepo kwenye mikutano.

6 Sasa zaidi ya wakati mwingine wote uliotangulia, ni lazima tushikilie kwa imara imani yetu na kuchochea wengine katika upendo na kazi njema. Ni lazima tuwe wenye juhudi katika jitihada zetu za kuhudhuria mikutano yote ya kundi. Hatutaki kuingia katika desturi au tabia ya kuacha kukusanyika pamoja. Twapaswa kufanya jitihada ya kudhamiria kutia moyo na kusaidia wengine, kutia ndani wahudhuriaji Ukumbusho, wawepo kwenye mikutano kwa ukawaida. Kwa njia hiyo, tutaonyesha upendo wetu kwa ajili ya wengine na uthamini wetu kwa ajili ya mikutano ya Kikristo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki