-
Iga Imani ya MusaMnara wa Mlinzi—2014 | Aprili 15
-
-
1, 2. (a) Musa alifanya uamuzi gani alipokuwa na umri wa miaka 40? (Tazama picha kwenye ukurasa huu.) (b) Kwa nini Musa alichagua kutendewa vibaya pamoja na watu wa Mungu?
MUSA alijua ufanisi ambao angepata nchini Misri. Aliona nyumba za kifahari za matajiri. Aliishi na familia ya kifalme. ‘Alifundishwa hekima yote ya Wamisri,’ ambayo huenda ilitia ndani sanaa, elimu ya nyota, hesabu, na mambo mengine ya kisayansi. (Mdo. 7:22) Angepata mali, mamlaka, na pendeleo ambalo Mmisri wa kawaida hangeweza kupata.
2 Hata hivyo, Musa alipokuwa na umri wa miaka 40 alifanya uamuzi ambao bila shaka ulimshangaza Farao na familia ya kifalme iliyomlea. Hakuchagua tu maisha ya Wamisri wa kawaida, badala yake alichagua kuishi na watumwa. Kwa nini? Musa alikuwa na imani. (Soma Waebrania 11:24-26.) Kwa imani, Musa hakuona tu ufanisi ambao angepata ulimwenguni. Kwa kuwa Musa alithamini mambo ya kiroho, alikuwa na imani katika Yehova, ‘Yule asiyeonekana,’ na katika utimizo wa ahadi Zake.—Ebr. 11:27.
-
-
Iga Imani ya MusaMnara wa Mlinzi—2014 | Aprili 15
-
-
6. (a) Kwa nini Musa alikataa “kuitwa mwana wa binti ya Farao”? (b) Kwa nini unafikiri kwamba Musa alifanya uamuzi unaofaa?
6 Imani ya Musa ilimsaidia pia kuamua jinsi atakavyotumia maisha yake. “Kwa imani Musa, alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti ya Farao.” (Ebr. 11:24) Musa hakujitetea kwamba angemtumikia Mungu akiwa katika makao ya mfalme na kutumia mali na mapendeleo yake kuwasaidia ndugu zake Waisraeli. Badala yake, Musa aliazimia kumpenda Yehova kwa moyo wake wote, nafsi yake yote, na nguvu zake zote. (Kum. 6:5) Uamuzi wa Musa ulimlinda kutokana na maumivu mengi ya moyo. Mwishowe, Waisraeli ndio waliochukua hazina nyingi za Misri alizoacha. (Kut. 12:35, 36) Farao aliaibishwa na kuuawa. (Zab. 136:15) Lakini Musa alitumiwa na Mungu kuliongoza taifa zima la Israeli mahali salama. Maisha yake yalikuwa na kusudi kwelikweli.
-