-
“Ulimwengu Haukustahili Kuwa Nao”Mnara wa Mlinzi—1987 | Januari 15
-
-
7. (a) Ni nani ambao “kupitia imani walishinda falme katika pambano”? (b) Ni nani ambao “walitekeleza uadilifu” kupitia imani?
7 Kwa imani sisi tunaweza kukabili kwa mafanikio kila jaribu la ukamilifu na tunaweza kufanya jambo lo lote linalopatana na mapenzi ya Mungu. (Soma Waebrania 11:33, 34, NW.) Kwa kutaja tu vitendo zaidi vya imani, inaonekana kwamba Paulo alikuwa akifikiria waamuzi, wafalme, na manabii Waebrania, kwa maana kitambo kidogo tu alikuwa ametoka kusema juu ya wanaume hao. “Kupitia imani” waamuzi hao kama Gideoni na Yeftha “walishinda falme katika pambano.” Ndivyo pia alivyofanya Mfalme Daudi, ambaye alitiisha Wafilisti, Wamoabi, Washami, Waedomi, na wengine. (2 Samweli 8:1-14) Pia kupitia imani, waamuzi wanyofu “walitekeleza uadilifu,” na mashauri yenye uadilifu ya Samweli na manabii wengine yalivuta mioyo ya angalau watu fulani waepuke au waache kutenda mabaya.—1 Samweli 12:20-25; Isaya 1:10-20.
-
-
“Ulimwengu Haukustahili Kuwa Nao”Mnara wa Mlinzi—1987 | Januari 15
-
-
10. Ni nani ambao ‘walizuia kani ya moto’ kupitia imani, na imani inayolinganika na hiyo itatuwezesha sisi tufanye nini?
10 Shadraka, Meshaki, na Abednego, Waebrania washika-ukamilifu washiriki wa Danieli, ni kama kweli “walizuia kani ya moto.” Walipotishwa na kifo katika tanuri iliyopashwa moto zaidi ya kawaida, wao walimwambia Mfalme Nebukadreza, kwamba Mungu wao angewaokoa au la, wao hawangetumikia miungu ya mfalme huyo Mbabuloni wala hawangeabudu mfano aliokuwa amesimamisha. Yehova hakuzima moto katika tanuri hiyo. lakini alihakikisha kwamba haukuwadhuru hata kidogo Waebrania hao watatu, (Danieli 3:1-30) Imani inayolinganika na hiyo inatuwezesha sisi tudumishe ukamilifu kwa Mungu kufikia hatua ya kuweza kuuawa mikononi mwa adui.—Ufunuo 2:10.
11. (a) Kupitia imani, ni nani ambao “waliokoka ncha ya upanga”? (b) Ni nani ambao “walifanywa wenye nyingi” kupitia imani (c) Ni nani ambao “wakawa wenye ushujaa katika vita” na ‘wakashinda na kukimbiza majeshi ya wageni’?
11 Daudi ‘aliokoka ncha ya upanga’ wa wanaume wa Mfalme Sauli. (1 Samweli 19:9-17) Manabii Eliya na Elisha pia waliokoka kifo cha upanga. (1 Wafalme 19:13; 2 Wafalme 6:11-23) Lakini ni nani ambao ‘kutoka hali ya udhaifu walifanywa wenye nguvu nyingi kupitia imani’? Basi, Gideoni alijihesabu yeye mwenyewe na wanaume wake kuwa dhaifu mno wasiweze kuokoa Israeli kutoka kwa Wamidiani. Lakini yeye ‘alifanywa mwenye nguvu nyingi’ na Mungu, ambaye alimpa ushindi—tena akiwa na wanaume 300 tu!—Waamuzi 6:14-16; 7:2-7, 22) Samsoni ‘alifanywa mwenye nguvu nyingi’ na Yehova ‘kutoka hali ya udhaifu’ wakati nywele zake zilipokatwa, naye akaua Wafilisti wengi. (Waamuzi 16:1921, 28-30; linganisha Waamuzi 15:13-19.) Huenda pia Paulo akawa alifikiri juu ya Mfalme Hezekia kuwa mmoja ‘aliyefanywa mwenye nguvu nyingi’ kutoka hali ya udhaifu kijeshi na hata kimwili. (Isaya 37:1–38:22) Miongoni mwa watumishi wa Mungu ambao “wakawa wenye ushujaa katika vita” walikuwa Mwamuzi Yeftha na Mfalme Daudi. (Waamuzi 11:32, 33; 2 Samweli 22:1, 2, 30-38) Na wale ambao ‘walishinda na kukimbiza majeshi ya kigeni’ ni kutia ndani mwamuzi Baraki. (Waamuzi 4:14-16) Matendo yote hayo hodari yanapasa yatusadikishe sisi kwamba kwa imani tunaweza kukabili kwa mafanikio kila jaribu la ukamilifu wetu na tunaweza kufanya jambo lo lote linalopatana na mapenzi ya Yehova.
-