Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Imarisha Imani Yako Kuhusu Mambo Unayotumaini
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2016 | Oktoba
    • 10. Tuna mifano gani ya watumishi wa Mungu waliokataa kuvunja utimilifu wao, na ni nini kilichowapa nguvu za kufanya hivyo?

      10 Kwenye Waebrania sura ya 11, mtume Paulo anaeleza kuhusu majaribu ambayo watumishi wengi wa Mungu walivumilia ingawa hataji majina yao. Kwa mfano, mtume huyo anataja wanawake wenye imani ambao walifiwa na wana wao, lakini baadaye waliwapokea kupitia ufufuo. Kisha anataja wengine ambao “hawakukubali kuachiliwa huru kupitia fidia fulani, ili waupate ufufuo ulio bora.” (Ebr. 11:35) Ingawa hatuwezi kuwa na uhakika Paulo alikuwa akizungumzia nani hasa, watu fulani kama vile Nabothi na Zekaria, walipigwa mawe hadi wakafa kwa sababu ya kumtii Mungu na kufanya mapenzi yake. (1 Fal. 21:3, 15; 2 Nya. 24:20, 21) Ni wazi kwamba Danieli na waandamani wake walikuwa na nafasi ya “[kukubali] kuachiliwa huru” ikiwa wangevunja utimilifu wao. Badala yake, waliamini uwezo wa Mungu na hilo liliwawezesha ‘kuziba vinywa vya simba’ na ‘kuzuia nguvu za moto’ kwa njia ya mfano.—Ebr. 11:33, 34; Dan. 3:16-18, 20, 28; 6:13, 16, 21-23.

  • Imarisha Imani Yako Kuhusu Mambo Unayotumaini
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2016 | Oktoba
    • 12. Ni nani aliyeweka mfano bora zaidi wa kuvumilia majaribu, na ni nini kilichomsaidia kufanya hivyo?

      12 Baada ya kueleza kuhusu wanaume na wanawake mbalimbali wenye imani, Paulo alizungumzia mfano bora zaidi wa imani, yaani, Bwana wetu Yesu Kristo. Andiko la Waebrania 12:2 linasema hivi: “Kwa ajili ya shangwe iliyowekwa mbele yake, yeye alivumilia mti wa mateso, akaidharau aibu, naye ameketi kwenye mkono wa kuume wa kiti cha ufalme cha Mungu.” Kwa kweli, tunapaswa ‘kufikiria sana’ mfano bora wa imani ambao Yesu alionyesha alipokabili lile jaribu kali zaidi. (Soma Waebrania 12:3.) Wakristo wa mapema waliokufa kwa sababu ya imani yao, kama vile mwanafunzi Antipa, walimwiga Yesu kwa kutovunja utimilifu wao. (Ufu. 2:13) Wakristo hao wangepata thawabu ya kufufuliwa ili waishi mbinguni, na hivyo kupokea ufufuo bora zaidi ya “ufufuo ulio bora” ambao wanaume wa zamani wenye imani walitazamia kupata. (Ebr. 11:35) Muda mfupi baada ya Ufalme kuanza kutawala katika mwaka wa 1914, watiwa mafuta hao waaminifu, ambao walikuwa wamelala usingizi katika kifo, walifufuliwa na kupewa uhai wa kiroho mbinguni ili wajiunge na Yesu katika kuwatawala wanadamu.—Ufu. 20:4.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki