Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Ulimwengu Haukustahili Kuwa Nao”
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Januari 15
    • 13. (a) “Ni nani waliopatwa na dhihaka na mapigo ya mijeledi”? (b) Ni nani waliopatwa na “vifungo na magereza”?

      13 Ikiwa sisi tuna imani tutaweza kuvumilia mateso. (Soma Waebrania 11:36-38, NW.) Tunapoteswa inasaidia kulikumbuka tumaini la ufufuo na kung’amua kwamba Mungu anaweza kututegemeza kama alivyofanyia “wengine [ambao] walipokea jaribu lao [au jaribu la imani] Kwa dhihaka na mapigo ya mijeledi. ndiyo, zaidi ya hilo, kwa vifungo na magereza.” wafanyia dhihaka manabii wake, mpaka hasira kali ya Yehova ikapanda dhidi ya watu wake.” (2 Nyakati 36:15.16, NW) Kwa imani, Mikaya. Elisha, na watumishi wengine wa Mungu walivumilia “dhihaka.” (1 Wafalme 22:24; Wafalme 2:23, 24; Zaburi 42:3) “Mapigo ya mijeledi” yalijulikana katika siku za wafalme na manabii wa Israeli, na. wapinzani ‘walimpiga dharuba’ Yeremia, si kumpiga kofi tu kwa uchokozi. “Vifungo na magereza” vinaweza kutukumbusha juu ya mambo yaliyompata na pia yaliyopata manabii Mikaya na Hanani. (Yeremia 20:1, 2; 37:15; 1 Wafalme 12:11; 22:26, 27; 2 Nyakati 16:7, 10) Kwa sababu ya kuwa na imani inayofanana na hiyo, mashahidi wa kisasa wa Yehova wameweza kuvumilia taabu zinazolinganika na hizo “kwa ajili ya uadilifu.”—1 Petro 3:14, NW.

  • “Ulimwengu Haukustahili Kuwa Nao”
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Januari 15
    • 15. Ni nani waliopatwa na “kutendwa vibaya” na “walitangatanga katika majangwa”?

      15 Wengine “walikufa kwa kuchinjwa kwa upanga,” kwa mfano, manabii wa Mungu wenzi wa Eliya ‘waliuawa kwa upanga’ katika siku za Mfalme Ahabu mwovu. (1 Wafalme 19:9, 10) Eliya na Elisha walikuwa miongoni mwa wale wenye imani ambao “walienda huku na huku katika ngozi za kondoo, katika ngozi za mbuzi, wao walipokuwa katika uhitaji, katika dhiki, chini ya kutendwa vibaya.” (1 Wafalme 19:5-8, 19; 2 Wafalme 1:8; 2:13; linganisha Yeremia 38:6.) Wale ambao “walitangatanga katika majangwa na milima na mapango na matundu ya dunia” wakiwa vitu vya mateso lazima wawe ni kutia ndani si Eliya na Elisha tu bali pia wale manabii 100 ambao Obadia alificha katika pango wakiwa hamsini-hamsini, akiwapa mkate na maji wakati Malkia Yezebeli mwabudu sanamu alipoanza ‘kuua manabii wa Yehova.’ (1 Wafalme 18:4, 13; 2 Wafalme 2:13; 6:13, 30, 31) Lo, washika-ukamilifu walioje! Si ajabu Paulo alisema: “Ulimwengu [jamii ya kibinadamu isiyo na uadilifu] haukustahili kuwa nao”!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki