-
ImaniUfahamu wa Kina wa Maandiko
-
-
Lakini imani ni muhimu sana, kwa sababu kukosa imani ni ‘dhambi ambayo humtatanisha mtu kwa urahisi.’ Ili kudumisha imani yenye nguvu ni lazima tufanye pigano kali kwa ajili ya imani, tuwapinge watu ambao hutumbukiza wengine katika uasherati, tupambane na matendo ya mwili, tuepuke mtego wa kupenda mali, tuepuke falsafa na mapokeo ya wanadamu yanayovunja imani, na zaidi ya yote, ‘tumtazame kwa makini Wakili Mkuu na Mkamilishaji wa imani yetu, Yesu.’—Ebr 12:1, 2; Yud 3, 4; Gal 5:19-21; 1Ti 6:9, 10; Kol 2:8.
-
-
Michezo Katika Nyakati za BibliaMnara wa Mlinzi—2006 | Machi 1
-
-
Mifano Iliyotokana na Michezo
Paulo na Petro walitumia vizuri mambo fulani ya michezo hiyo ili kufundisha kwa mifano. Tofauti na tuzo ambalo washindanaji walijitahidi kushinda katika michezo ya Ugiriki, taji ambalo Mkristo mtiwa-mafuta hujitahidi kupata, si la majani yanayoharibika, bali ni zawadi ya uhai usioweza kufa. (1 Petro 1:3, 4; 5:4) Mkristo huyo alipaswa kukimbia akiwa na nia ya kushinda tuzo hilo naye alipaswa kulikazia macho. Kutazama nyuma kungekuwa hatari. (1 Wakorintho 9:24; Wafilipi 3:13, 14) Mkristo huyo alipaswa kushindana kulingana na sheria za maadili ili asiondolewe kwenye mashindano. (2 Timotheo 2:5) Alipaswa ajizuie, ajitie nidhamu, na kufanya mazoezi. (1 Wakorintho 9:25; 1 Petro 5:10) Jitihada za Mkristo huyo zilipaswa kuelekezwa mahali panapofaa huku akifikiria ushindi, kama vile ngumi za mpiganaji aliyezoezwa vizuri zinavyokuwa na matokeo zinapolenga shabaha; ingawa pigano la Mkristo si dhidi ya mwanadamu mwenzake, bali dhidi ya vitu, kutia ndani vile vilivyo ndani yake, ambavyo vinaweza kumfanya asifaulu. (1 Wakorintho 9:26, 27; 1 Timotheo 6:12) Mkristo huyo alipaswa kuondoa kila uzito unaoweza kumzuia na vilevile dhambi inayotatanisha ya kukosa imani, sawa na vile washindanaji katika mbio walivyovua mavazi mazito. Mkimbiaji Mkristo alipaswa kujitayarisha kwa ajili ya mbio zinazohitaji uvumilivu, bali si kukimbia kasi kwa muda mfupi.—Waebrania 12:1, 2.
Kwenye Waebrania 12:1, Paulo anazungumza kuhusu ‘wingu kubwa la mashahidi [Kigiriki, mar·tyʹron] linalotuzunguka.’ Sura inayotangulia inaonyesha wazi kwamba Paulo hazungumzi kuhusu umati wa watazamaji. Paulo anairejelea sura hiyo kwa kusema, “Kwa hiyo, basi, . . . ” Hivyo, Paulo anawatia moyo Wakristo waendelee katika mbio kwa kuwaonyesha mifano bora ya wengine ambao walikuwa wakimbiaji wala si watazamaji, naye anawahimiza wamtazame kwa makini yule ambaye tayari alikuwa ameshinda na ambaye sasa ni Hakimu wao, yaani, Kristo Yesu.
-