-
Toa Ushahidi kwa Ajili ya Yehova na UsichokeMnara wa Mlinzi—1989 | Desemba 15
-
-
8. (a) Ni nini kilichomsukuma Paulo awaandikie Waebrania barua yake? (b) Twataka kukaza fikira zetu upande gani wa barua yake, na kwa nini?
8 Katika 61 W.K. hivi, Paulo alitiwa gerezani katika Roma, lakini yeye alijua kilichokuwa kikitendeka kwa ndugu zake katika Yerusalemu. Basi, chini ya mwongozo wa roho ya Yehova, aliwaandikia Waebrania barua yake ya wakati ufaao. Imejaa hangaiko la upendo kwa ndugu na dada zake Waebrania. Paulo alijua walichohitaji ili imani na tumaini lao litiwe nguvu katika Yehova akiwa Msaidiaji wao. Ndipo wangeweza ‘kupiga mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yao’ na kusema hivi kwa uthabiti: “Yehova ndiye msaidiaji wangu; mimi sitaogopa. Mwanadamu aweza kunifanya nini?” (Waebrania 12:1; 13:6, NW) Sasa twataka kukazia fikira zetu upande huu wa barua ya Paulo kwa Waebrania (sura za 11-13). Kwa nini? Kwa sababu hali iliyokabili Wakristo hao wa mapema ndiyo ile ile yenye kukabili Mashahidi wa Yehova leo.
-
-
Toa Ushahidi kwa Ajili ya Yehova na UsichokeMnara wa Mlinzi—1989 | Desemba 15
-
-
11. Sisi leo twaweza kunufaikaje na “wingu kubwa sana la mashahidi kuzunguka sisi”?
11 Baada ya masimulizi ambayo yahusu wanaume na wanawake hawa waaminifu, Paulo asema: “Hivyo, basi, kwa sababu sisi tuna wingu kubwa sana la mashahidi kuzunguka sisi, acheni sisi pia tuvue kila uzito na dhambi ambayo hutatanisha sisi kwa urahisi, na acheni sisi tukimbie kwa uvumilivu katika shindano la mbio ambalo limewekwa mbele yetu sisi.” (Waebrania 12:1, NW) Ingawa sasa wamelala kaburini, je! mashahidi hawa waaminifu waliokuwa kielelezo wako hai katika akili yetu? Je! wewe unawajua wao vizuri pamoja na mambo yaliyowapata hivi kwamba waweza kujibu ndiyo? Hii ni mojapo ya thawabu nyingi za funzo la Biblia la ukawaida, kutumia hisi zetu zote kukumbuka mambo ya kusisimua yaliyopata hili “wingu kubwa sana la mashahidi.” Kweli kweli, kuzingatia kielelezo chao cha uaminifu kutatusaidia sana tushinde ukosefu wowote wa imani. Kutatusaidia sisi nasi tutoe ushahidi wenye ujasiri na kutokuhofu kuhusu ukweli chini ya hali zote. —Warumi 15:4.
-