-
Uvumilivu—Muhimu kwa WakristoMnara wa Mlinzi—1993 | Septemba 15
-
-
17. (a) Yesu alivumilia majaribu gani? (b) Kule kuteseka kwingi ambako Yesu alivumilia kwaweza labda kuonwa kutokana na jambo gani? (Ona kielezi-chini.)
17 Biblia yatuhimiza ‘tumtazame kwa mkazo’ Yesu na ‘kumfikiria kwa ukaribu.’ Yeye alivumilia majaribu gani? Baadhi yayo yalitokana na dhambi na kutokamilika kwa wengine. Yesu alivumilia ‘maongezi-kinyume yenye kufanywa na watenda dhambi’ na pia matatizo yaliyotokea miongoni mwa wanafunzi wake, kutia ndani mabishano yao ya mara kwa mara juu ya ni nani aliyekuwa mkuu zaidi. Zaidi ya hayo, alikabili mtihani wa imani usio na kifani. ‘Alivumilia mti wa mateso.’ (Waebrania 12:1-3, NW; Luka 9:46; 22:24) Ni vigumu hata kuwazia kule kuteseka kiakili na kimwili kulikohusika katika maumivu ya kutundikwa na ile aibu ya kuuawa akiwa mkufuru.a
18. Kulingana na mtume Paulo, ni mambo gani mawili yaliyomtegemeza Yesu?
18 Ni nini kilichomwezesha Yesu avumilie hadi mwisho? Mtume Paulo ataja mambo mawili yaliyomtegemeza Yesu: “maombi na dua” na pia “furaha iliyowekwa mbele yake.” Yesu, yule Mwana mkamilifu wa Mungu, hakuona aibu kuomba msaada. Alisali “pamoja na kulia sana na machozi.” (Waebrania 5:7; 12:2) Hasa wakati jaribu lake kuu zaidi lilipokuwa likikaribia ndipo aliona ni lazima kusali mara kwa mara na kwa bidii ili kupata nguvu. (Luka 22:39-44) Kwa kuitikia maombi ya Yesu, Yehova hakuliondoa lile jaribu, bali alimwimarisha Yesu kulivumilia. Yesu alivumilia pia kwa sababu alitazama ng’ambo ya mti wa mateso hadi kwenye thawabu yake—ile furaha ambayo angekuwa nayo katika kuchangia utakaso wa jina la Yehova na kufidiwa kwa familia ya kibinadamu kutoka katika kifo.—Mathayo 6:9; 20:28.
-
-
Uvumilivu—Muhimu kwa WakristoMnara wa Mlinzi—1993 | Septemba 15
-
-
20 Nyakati fulani ni lazima tuvumilie kwa machozi. Kwa Yesu maumivu ya mti wa mateso hayakuwa sababu hasa ya kushangilia. Badala ya hivyo, furaha ilikuwa katika ile thawabu iliyowekwa mbele yake. Katika hali yetu si jambo halisi kutazamia kwamba sikuzote tutahisi uchangamfu na msisimuko tunapokuwa chini ya jaribu. (Linganisha Waebrania 12:11.) Hata hivyo, kwa kutazama mbele kwenye thawabu, huenda tukaweza ‘kuhesabu ya kuwa ni furaha tupu’ hata tunapokabili hali zenye kujaribu zaidi. (Yakobo 1:2-4; Matendo 5:41) Jambo la maana ni kwamba tuendelee kuwa thabiti—hata ikiwa ni lazima iwe kwa machozi. Kwa vyovyote vile, Yesu hakusema, ‘Mwenye kulia machozi machache zaidi, ndiye atakayeokoka’ bali, “Mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.”—Mathayo 24:13.
-