Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nidhamu Inayoweza Kuzaa Tunda Lenye Kuamanika
    Mnara wa Mlinzi—1988 | Aprili 15
    • “Hakuna nidhamu ambayo inaonekana kwa wakati uliopo kuwa yenye shangwe, bali yenye kihoro; hata hivyo baadaye kwa wale ambao wamezoezwa nayo inazaa tunda lenye kuamanika, yaani, uadilifu.”​—WAEBRANIA 12:11, NW.

      1, 2. (a) Kulingana na Waebrania 12:9-11, Mungu anaandaa nini kwa upendo? (b) Ni nini kielelezo kimoja cha nidhamu, na ni jambo gani ambalo linaweza kutokana nayo?

      FIKIRI nyuma kwenye siku za utoto wako. Je! wewe unaweza kukumbuka wazazi wako wakikutia nidhamu? Walio wengi kati yetu tunaweza kukumbuka. Mtume Paulo alitumia hicho kama kielezi wakati alipokuwa akieleza juu ya nidhamu kutoka kwa Mungu, kama tunavyosoma katika Waebrania 12:9-11.

      2 Nidhamu ya Mungu iliyo kama ya baba, ambayo inaweza kuathiri maisha zetu za kiroho, inaweza kuwa ya namna nyingi. Moja ni mpango wake wa kuweka nje ya kundi la Kikristo mtu ambaye hataki tena kuishi kwa kutimiza viwango vya Mungu au anakataa kufanya hivyo. Mtu ambaye anaadhibiwa au kutiwa nidhamu kwa ukali hivyo huenda akatubu na kugeuka. Anapokuwa akitendewa hivyo, kundi la washikamanifu linatiwa nidhamu pia katika jambo la kwamba wao wanajifunza umaana wa kujifanyiza kulingana na viwango vya juu vya Mungu.​—1 Timotheo 1:20.

  • Nidhamu Inayoweza Kuzaa Tunda Lenye Kuamanika
    Mnara wa Mlinzi—1988 | Aprili 15
    • Kwa Sababu Gani Msimamo Huu Thabiti?

      4. Mara kwa mara ni jambo gani ambalo linatukia kwa wengine katika kundi? (Wagalatia 6:1; Yuda 23)

      4 Walio wengi wa Wakristo wa kweli wanaunga mkono kwa ushikamanifu Mungu na sheria zake za uadilifu. (1 Wathesalonike 1:2-7; Waebrania 6:10) Ingawa hivyo mara kwa mara mtu fulani anakengeuka kutoka kile kijia cha ukweli. Mathalani, ajaposaidiwa na wazee Wakristo, huenda yeye akavunja sheria za Mungu kwa kutotubu. Au huenda yeye akakataa ile imani kwa kufundisha fundisho lisilo la kweli au kwa kujitenga mwenyewe na ushirika wa kundi. Basi ni jambo gani linalopasa kufanywa? Mambo kama hayo yalitukia hata wakati mitume walipokuwa hai; kwa sababu hiyo, acheni tuone wao waliandika nini juu ya hilo.

      5, 6. (a) Sisi tuna mashauri gani ya hekima kwa habari ya kushughulika na wale wanaotenda dhambi nzito na hawaonyeshi toba? (Mathayo 18:17) (b) Ni maswali gani ambayo sisi tunaelekeana nayo?

      5 Wakati mwanamume mmoja katika Korintho alipokuwa mkosefu wa adili kwa kutotubu, Paulo aliambia lile kundi: “Ninyi mwache kabisa kuchangamana katika ushirika pamoja na ye yote anayeitwa ndugu ambaye ni mwasherati au mtu mwenye pupa au mwabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyakuzi, hata msiwe mnakula pamoja na mtu huyo.” (1 Wakorintho 5:11-13, NW) Jambo ilo hilo lilipasa kutukia kwa waasi-imani, kama vile Himenayo: “Kwa habari ya binadamu anayeendeleza farakano, mkatae baada ya onyo la upole la kwanza na la pili; ukijua kwamba mtu kama huyo ameondolewa katika njia ile na anafanya dhambi.” (Tito 3:10, 11; 1 Timotheo 1:19, 20, NW) Kuepukwa kabisa kwa namna hiyo kungefaa, pia, kwa mmoja ye yote ambaye analikataa kundi: “Wao walitoka kati yetu, lakini wao hawakuwa wa aina yetu; maana kama wao wangalikuwa wa aina yetu, wangaliendelea kuwa pamoja nasi. Lakini wao walienda nje kwamba iweze kuonyeshwa wazi kwamba si wote ambao wamekuwa wa aina yetu.”​—1 Yohana 2:18, 19, NW.

      6 Inatumainiwa sana kwamba mtu wa namna hii atatubu ili kwamba yeye aweze kukubaliwa tena. (Matendo 3:19) Lakini kwa sasa, je! Wakristo wawe na ushirika wa kiasi pamoja naye, au inahitajiwa kabisa kumwepuka mtu huyo vilivyo? Ikiwa ndivyo, kwa sababu gani?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki