-
Maoni ya Biblia Kuhusu Pesa na KaziFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
2. Biblia inasema nini kuhusu pesa?
Biblia inasema ‘pesa ni ulinzi,’ lakini pia inatuonya kwamba pesa peke yake haziwezi kutuletea furaha. (Mhubiri 7:12) Basi tunatiwa moyo tusipende pesa bali ‘turidhike na vitu tulivyo navyo.’ (Soma Waebrania 13:5.) Tunaporidhika na vitu tulivyo navyo, tunaepuka mahangaiko ya kutafuta vitu vingi zaidi. Tunaepuka madeni yasiyo ya lazima. (Methali 22:7) Na tunaepuka hatari ya kucheza kamari au kunaswa na njia za kupata utajiri wa haraka.
-
-
Maoni ya Biblia Kuhusu Pesa na KaziFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
5. Tunanufaika tunaporidhika
Watu wengi hujitahidi kutafuta pesa nyingi iwezekanavyo. Lakini Biblia inatoa ushauri tofauti. Soma 1 Timotheo 6:6-8, kisha mzungumzie swali hili:
Biblia inatutia moyo tufanye nini?
Tunaweza kuwa na furaha hata tukiwa na vitu vichache sana. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.
Ingawa familia hizo hazina pesa nyingi, kwa nini wana furaha?
Namna gani ikiwa tuna vitu vingi na bado tunatamani kupata vingi zaidi? Yesu alitoa mfano unaoonyesha hatari ya kufanya hivyo. Soma Luka 12:15-21, kisha mzungumzie swali hili:
Umejifunza nini kutokana na mfano wa Yesu?—Ona mstari wa 15.
Soma na ulinganishe Methali 10:22 na 1 Timotheo 6:10. Kisha mzungumzie maswali haya:
Unafikiri ni jambo gani lililo muhimu zaidi? Kuwa rafiki ya Yehova, au kuwa na pesa nyingi sana? Kwa nini?
Ni matatizo gani yanayosababishwa na kutafuta pesa nyingi zaidi?
-