-
Yehova Ndiye Msaidiaji WanguMnara wa Mlinzi—1989 | Desemba 15
-
-
1, 2. (a) Mtunga zaburi na mtume Paulo walionyesha uhakika gani katika Yehova? (b) Ni maswali gani ambayo yazuka?
YEHOVA MUNGU ni chanzo kisichoshindwa cha msaada. Mtunga zaburi alijua jambo hili kutokana na mambo yaliyompata naye angeweza kusema: “Yehova yuko upande wangu, mimi sitaogopa. Mwanadamu wa dunia aweza kunifanya nini?” (Zaburi 118:6, NW) Mawazo ya moyoni yaliyo kama hayo yalielezwa na mtume Paulo alipowaandikia Wakristo Waebrania barua yake iliyovuviwa kimungu.
2 Yaelekea akinukuu maneno ya mtunga zaburi kutoka Septuagint ya Kigiriki, Paulo aliwaambia waabudu wenzi Waebrania: ‘Mwe wenye moyo mkuu na kusema: “Yehova ndiye msaidiaji wangu; mimi sitaogopa. Mwanadamu aweza kunifanya nini?”’ (Waebrania 13:6, NW) Kwa nini mtume aliandika kwa njia hii? Nasi twaweza kujifunza nini kutokana na habari zenye kuzunguka mstari huu?
Katika Uhitaji wa Kutaka Msaada wa Yehova
3. (a) Yehova alithibitika kuwa Msaidiaji wa Paulo chini ya hali gani? (b) Kwa nini Wakristo Waebrania hasa walihitaji Yehova awe Msaidiaji wao?
3 Paulo alikuwa shahidi mwenye kujidhabihu aliyekuwa na ushuhuda wa kuthibitisha kwamba Yehova alikuwa Msaidiaji wake. Mungu alimsaidia mtume alipokabili magumu mengi. Paulo alikuwa amewekwa gerezani, akachapwa, na kupigwa kwa mawe. Alivunjikiwa merikebu na pia akapatwa na hatari nyingine nyingi katika safari zake akiwa mhudumu Mkristo. Alijua sana kutoa jasho, kukosa usingizi usiku, njaa, kiu, na hata uchi. “Baghairi ya mambo ya nje,” akasema, “yako yanijiayo kila siku, ndiyo maangalizi ya makanisa [makundi, NW] yote.” (2 Wakorintho 11:24-29) Paulo aliwahangaikia hivyo Wakristo Waebrania. Siku za Yerusalemu zilikuwa zimepunguzwa, na ndugu na dada Wayahudi wa mtume huyo waliokuwa Yudea wangekabili mitihani mikubwa ya imani. (Danieli 9:24-27; Luka 21:5-24) Kwa hiyo wangehitaji kuwa na Yehova akiwa Msaidiaji wao.
-
-
Yehova Ndiye Msaidiaji WanguMnara wa Mlinzi—1989 | Desemba 15
-
-
20. (a) Ni nini andiko la mwaka wa 1990? (b) Twapaswa tuendelee kufanya nini bila woga?
20 Msaada wa Mungu usioshindwa utakaziwa miongoni mwa Mashahidi wa Yehova katika miezi iliyo mbele, kwa kuwa andiko lao la mwaka 1990 lasomwa hivi: ‘Mwe wenye moyo mkuu na kusema: ‘Yehova ndiye msaidiaji wangu.’ “Maneno haya yapatikana kwenye Waebrania 13:6, NW, ambapo Paulo alinukuu mtunga zaburi na akawaambia Waebrania hivi: “Ili tuwe wenye moyo mkuu na kusema: ‘Yehova ndiye msaidiaji wangu; mimi sitaogopa. Mwanadamu aweza kunifanya nini?”’ (Zaburi 118:6, NW) Ijapokuwa twanyanyaswa, hatuogopi, kwa kuwa wanadamu hawawezi kufanya zaidi ya yale ambayo Mungu aruhusu. (Zaburi 27:1) Hata tukilazimika kufa tukiwa tumeshika uaminifu wa kimaadili, tuna tumaini la ufufuo. (Matendo 24:15) Basi na tuendelee kumfuata Kiolezo wetu katika ‘kutoa utumishi mtakatifu tukiwa na hofu na kicho cha kimungu,’ tukiwa na uhakika kwamba Yehova ni Msaidiaji wetu.
-