Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kujitiisha kwa Unyenyekevu Chini ya Wachungaji Wenye Upendo
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Aprili 1
    • 7. Mtume Paulo alitoa shauri gani kuhusu mtazamo wetu kuelekea waangalizi Wakristo?

      7 Wachungaji wetu wa kimbingu, Yehova Mungu na Yesu Kristo, wanatutazamia tutii na kunyenyekea wachungaji hao wadogo ambao wamepewa majukumu kutanikoni. (1 Petro 5:5) Akiongozwa na roho ya Mungu, mtume Paulo aliandika hivi: “Wakumbukeni wale ambao wanaongoza katikati yenu, ambao wamelisema neno la Mungu kwenu, nanyi mnapotafakari jinsi mwisho wa mwenendo wao unavyokuwa, igeni imani yao. Watiini wale wanaoongoza katikati yenu na mnyenyekee, kwa maana wanaendelea kuzilinda nafsi zenu kama wale watakaotoa hesabu; ili wafanye hivyo kwa shangwe na si kwa kuugua, kwa maana kufanya hivyo kungewadhuru ninyi.”—Waebrania 13:7, 17.

      8. Paulo anatuomba ‘tutafakari’ nini, na tunapaswa ‘kutii’ tukiwa na mtazamo gani?

      8 Ona kwamba Paulo anatuomba ‘tutafakari,’ au kuchunguza kwa uangalifu, mwisho wa mwenendo wa uaminifu wa wazee na kuiga mifano hiyo ya imani. Kwa kuongezea, anatushauri tunyenyekee na kutii mwelekezo wa wanaume hao waliowekwa rasmi. Msomi mmoja wa Biblia anayeitwa R. T. France anaeleza kwamba katika Kigiriki cha awali, neno ambalo limetafsiriwa “watiini” si “neno la kawaida linalotumiwa kuhusiana na utii, lakini linamaanisha kihalisi ‘kusadiki,’ na linaonyesha kukubali uongozi wao kwa kupenda.” Tunawatii wazee si kwa sababu tu tunaagizwa tufanye hivyo katika Neno la Mungu, lakini pia kwa sababu tunasadiki kwamba wanahangaikia kabisa mambo ya Ufalme na hali yetu njema. Bila shaka, tutakuwa wenye furaha tukikubali uongozi wao kwa kupenda.

  • Kujitiisha kwa Unyenyekevu Chini ya Wachungaji Wenye Upendo
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Aprili 1
    • 10, 11. Waangalizi “wamelisema neno la Mungu” jinsi gani kwa Wakristo wenzao katika karne ya kwanza na leo?

      10 Katika andiko la Waebrania 13:7, 17 linalotajwa hapo juu, mtume Paulo anatoa sababu nne zinazoonyesha kwa nini tunapaswa kunyenyekea na kuwatii waangalizi Wakristo. Sababu ya kwanza ni kwamba “wamelisema neno la Mungu” kwetu. Kumbuka kwamba Yesu anatoa kwa kutaniko “zawadi katika wanadamu” kwa kusudi la “kuwarekebisha upya watakatifu.” (Waefeso 4:11, 12) Alirekebisha upya fikira na mwenendo wa Wakristo wa karne ya kwanza kupitia wachungaji waaminifu walio chini yake. Wengine wao waliongozwa na roho ya Mungu kuandika barua kwa makutaniko. Aliwatumia waangalizi hao waliowekwa rasmi na roho kuwaongoza na kuwajenga Wakristo wa mapema.—1 Wakorintho 16:15-18; 2 Timotheo 2:2; Tito 1:5.

      11 Leo, Yesu anatuelekeza kupitia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” anayewakilishwa na Baraza lake Linaloongoza na wazee waliowekwa rasmi. (Mathayo 24:45) Tunatii shauri hili la Paulo kwa kuwa tunamheshimu “mchungaji mkuu,” Yesu Kristo: “Mwatilie maanani wale wanaofanya kazi kwa bidii kati yenu na kuwasimamia ninyi katika Bwana na kuwaonya ninyi.”—1 Petro 5:4; 1 Wathesalonike 5:12; 1 Timotheo 5:17.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki