Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Toeni Dhabihu Ambazo Zampendeza Yehova
    Mnara wa Mlinzi—1989 | Desemba 15
    • 1. Yehova aliwahimiza Waisraeli watenda dhambi wafanye nini?

      YEHOVA ndiye Msaidiaji wa wale wanaomtolea dhabihu zenye kukubalika. Basi, wakati mmoja upendeleo wake ulikuwa juu ya Waisraeli waliotoa dhabihu za wanyama. Lakini ni nini kilichotukia walipotenda dhambi kwa kurudiarudia? Kupitia nabii Hosea, wao walihimizwa hivi: “Ee Israeli, mrudie Bwana [Yehova, NW], Mungu wako; maana umeanguka kwa sababu ya uovu wako. Chukueni maneno pamoja nanyi, mkamrudie Bwana [Yehova]; mkamwambie, Ondoa maovu yote, uyatakabali yaliyo mema; na hivyo ndivyo tutakavyotoa sadaka za midomo yetu kana kwamba ni ng’ombe [ng’ombe ndume wachanga, NW ].’”—Hosea 14:1, 2.

      2. ‘Ng’ombe wa midomo’ walikuwa nini, na mtume Paulo alitajaje kijuu-juu unabii wa Hosea?

      2 Hivyo ndivyo watu wa kale wa Mungu walivyotiwa moyo wamtolee Yehova Mungu ‘sadaka za midomo yao kana kwamba ni ng’ombe.’ Hizo zilikuwa nini? Dhabihu za sifa ya moyo mweupe! Akitaja kijuu-juu unabii huu, mtume Paulo aliwahimiza Wakristo Waebrania ‘wamtolee Mungu dhabihu ya sifa, yaani, lile tunda la midomo ambayo hufanya julisho la peupe kwa jina lake.’ (Waebrania 13:15, NW) Ni nini kiwezacho kusaidia Mashahidi wa Yehova watoe dhabihu za namna hiyo leo?

  • Toeni Dhabihu Ambazo Zampendeza Yehova
    Mnara wa Mlinzi—1989 | Desemba 15
    • 13. Dhabihu ambazo hupendeza Mungu hazitii ndani nini tu?

      13 Ndipo Paulo akataja dhabihu ambazo zapendeza Mungu, akiandika hivi: “Kupitia kwake yeye [Yesu] na tumtolee Mungu siku-zote dhabihu ya kusifu, yaani, lile tunda la midomo ambayo hufanya julisho la peupe kwa jina lake. Tena, msisahau kutenda mema na kushiriki vitu pamoja na wengine, kwa maana Mungu anapendezwa sana na dhabihu kama hizo.” (Waebrania 13:15, 16, NW) Dhabihu za Kikristo hazitii ndani kazi za kufadhili wanadamu tu. Kwa ukawaida watu hufanya mambo hayo. Mathalani, jambo hili lilitukia wakati watu kutoka mataifa mengi walipokuja kuwasaidia majeruhi wa tetemeko la dunia katika Armenia ya Urusi mwishoni mwa mwaka 1988.

      14. Kumtolea Mungu dhabihu yenye kukubalika hukazia kazi gani?

      14 Msingi wa utumishi mtakatifu ambao sisi humtolea Yehova ‘tukiwa na hofu na kicho kwa Mungu’ ni aina ile ya upendo wa kujidhabihu ambao Yesu alionyesha. (Waebrania 12:28; Yohana 13:34; 15:13) Utumishi huu hukazia kazi yetu ya kuhubiri, kwa kuwa kupitia Kristo akiwa Kuhani Mkuu ‘twamtolea Mungu dhabihu ya kusifu, yaani, lile tunda la midomo ambayo hufanya julisho la peupe kwa jina lake.’ (Hosea 14:2; Warumi 10:10-15; Waebrania 7:26, NW) Bila shaka, hatusahau ‘kutenda mema na kushiriki vitu pamoja na wengine,’ hata kutia ndani wengine wasio wa “jamaa ya waaminio.” (Wagalatia 6:10) Hasa wakati Wakristo wenzi wapatwapo na afa au iwapo wana uhitaji au udhia, sisi twatoa msaada wenye upendo wa kimwili na kiroho. Kwa nini? Kwa sababu twapendana. Twataka wao pia waweze kushika julisho la peupe la tumaini lao bila kuyumba-yumba, “kwa maana Mungu anapendezwa sana na dhabihu kama hizo.”—Waebrania 10:23-25; Yakobo 1:27.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki