Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kujitiisha kwa Unyenyekevu Chini ya Wachungaji Wenye Upendo
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Aprili 1
    • 7. Mtume Paulo alitoa shauri gani kuhusu mtazamo wetu kuelekea waangalizi Wakristo?

      7 Wachungaji wetu wa kimbingu, Yehova Mungu na Yesu Kristo, wanatutazamia tutii na kunyenyekea wachungaji hao wadogo ambao wamepewa majukumu kutanikoni. (1 Petro 5:5) Akiongozwa na roho ya Mungu, mtume Paulo aliandika hivi: “Wakumbukeni wale ambao wanaongoza katikati yenu, ambao wamelisema neno la Mungu kwenu, nanyi mnapotafakari jinsi mwisho wa mwenendo wao unavyokuwa, igeni imani yao. Watiini wale wanaoongoza katikati yenu na mnyenyekee, kwa maana wanaendelea kuzilinda nafsi zenu kama wale watakaotoa hesabu; ili wafanye hivyo kwa shangwe na si kwa kuugua, kwa maana kufanya hivyo kungewadhuru ninyi.”—Waebrania 13:7, 17.

      8. Paulo anatuomba ‘tutafakari’ nini, na tunapaswa ‘kutii’ tukiwa na mtazamo gani?

      8 Ona kwamba Paulo anatuomba ‘tutafakari,’ au kuchunguza kwa uangalifu, mwisho wa mwenendo wa uaminifu wa wazee na kuiga mifano hiyo ya imani. Kwa kuongezea, anatushauri tunyenyekee na kutii mwelekezo wa wanaume hao waliowekwa rasmi. Msomi mmoja wa Biblia anayeitwa R. T. France anaeleza kwamba katika Kigiriki cha awali, neno ambalo limetafsiriwa “watiini” si “neno la kawaida linalotumiwa kuhusiana na utii, lakini linamaanisha kihalisi ‘kusadiki,’ na linaonyesha kukubali uongozi wao kwa kupenda.” Tunawatii wazee si kwa sababu tu tunaagizwa tufanye hivyo katika Neno la Mungu, lakini pia kwa sababu tunasadiki kwamba wanahangaikia kabisa mambo ya Ufalme na hali yetu njema. Bila shaka, tutakuwa wenye furaha tukikubali uongozi wao kwa kupenda.

      9. Mbali na kutii, kwa nini ni muhimu kwetu ‘kunyenyekea’?

      9 Namna gani ikiwa hatusadiki kwamba njia ambayo wazee wanatuelekeza tufanye jambo fulani ndiyo njia bora ya kufanya jambo hilo? Huo ndio wakati hasa tunapohitaji kunyenyekea. Ni rahisi kutii wakati kila jambo linaeleweka nasi tunakubaliana na uamuzi wao, lakini je, tutaonyesha kwamba kwa kweli sisi tunanyenyekea na kutii hata wakati ambapo sisi binafsi hatuelewi mwelekezo uliotolewa? Petro, ambaye alikuja kuwa mtume baadaye, alionyesha unyenyekevu wa aina hiyo.—Luka 5:4, 5.

  • Kujitiisha kwa Unyenyekevu Chini ya Wachungaji Wenye Upendo
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Aprili 1
    • 12. Waangalizi “wanaendelea kuzilinda nafsi [zetu]” kwa njia gani?

      12 Sababu ya pili inayotufanya tushirikiane na waangalizi Wakristo ni kwamba “wanaendelea kuzilinda nafsi [zetu].” Wakigundua katika mtazamo au mwenendo wetu jambo fulani ambalo linaweza kuhatarisha hali yetu ya kiroho, kwa haraka wanatupa shauri linalohitajiwa wakiwa na kusudi la kuturekebisha upya. (Wagalatia 6:1) Neno la Kigiriki linalotafsiriwa ‘kulinda’ linamaanisha kihalisi “kujinyima usingizi.” Msomi mmoja wa Biblia anasema kwamba neno hilo “linadokeza hali ya mchungaji ya kukaa macho daima.” Zaidi ya kukaa macho daima kiroho, huenda wazee wakakosa usingizi wakihangaikia hali yetu ya kiroho. Je, hatupaswi kushirikiana kwa kupenda na wachungaji hao wadogo wenye upendo, ambao wanafanya yote wanayoweza ili kuiga wororo wa Yesu Kristo, yule “mchungaji mkuu wa kondoo”?—Waebrania 13:20.

      13. Waangalizi na Wakristo wote watatoa hesabu kwa nani na kwa njia gani?

      13 Sababu ya tatu inayotufanya tushirikiane kwa kupenda na waangalizi ni kwamba wanatulinda “kama wale watakaotoa hesabu.” Waangalizi wanakumbuka kwamba wao ni wachungaji wadogo, wanaotumika chini ya Wachungaji wa kimbingu, Yehova Mungu na Yesu Kristo. (Ezekieli 34:22-24) Yehova ndiye Mmiliki wa kondoo, ambao ‘aliwanunua kwa damu ya Mwana wake mwenyewe,’ Naye atawatoza hesabu waangalizi waliowekwa rasmi kwa sababu ya jinsi wanavyolitendea kundi Lake, ambalo linapaswa kutendewa “kwa wororo.” (Matendo 20:28, 29) Kwa hiyo, sote tutatoa hesabu kwa Yehova kulingana na jinsi tunavyoitikia mwelekezo wake. (Waroma 14:10-12) Kuwatii wazee waliowekwa rasmi kunathibitisha pia kwamba tunamnyenyekea Kristo, Kichwa cha kutaniko.—Wakolosai 2:19.

      14. Ni nini kinachoweza kuwafanya waangalizi Wakristo ‘waugue,’ na matokeo yanaweza kuwa nini?

      14 Paulo alitaja sababu ya nne inayopaswa kutufanya tujitiishe kwa unyenyekevu chini ya waangalizi Wakristo. Aliandika hivi: “Ili wafanye hivyo kwa shangwe na si kwa kuugua, kwa maana kufanya hivyo kungewadhuru ninyi.” (Waebrania 13:17) Wazee Wakristo wana majukumu mazito sana kama vile kufundisha, kufanya uchungaji, kuongoza katika kazi ya kuhubiri, kutunza familia zao, na kushughulikia matatizo kutanikoni. (2 Wakorintho 11:28, 29) Tukikosa kushirikiana nao, tunafanya kazi yao iwe ngumu zaidi. Hilo litawafanya ‘waugue.’ Kuonyesha roho ya kutoshirikiana hakumpendezi Yehova na kunaweza kutudhuru. Lakini, tunapoonyesha heshima na ushirikiano unaofaa, wazee wanaweza kutimiza wajibu wao kwa shangwe, na hilo linachangia umoja na kutuletea sote shangwe tunaposhiriki katika kazi ya kuhubiri Ufalme.—Waroma 15:5, 6.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki