-
Je, Kuungama Dhambi Ni Takwa la Mungu?Mnara wa Mlinzi—2010 | Septemba 1
-
-
Tukirejelea tena kitabu cha Yakobo, tunapata maneno haya yenye kutia moyo: “Je, kuna yeyote mgonjwa [kiroho] kati yenu? Na awaite kwake wanaume wazee wa kutaniko, nao wasali juu yake, wakimpaka mafuta katika jina la Yehova. Na sala ya imani itamponya huyo asiyejisikia vizuri, na Yehova atamwinua. Pia, ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.”—Yakobo 5:14, 15.
Kwa mara nyingine tena, wanaume wazee, au wazee, wanahimizwa washughulikie mahitaji ya kondoo. Jinsi gani? Si kwa kumsikiliza tu mtu anapoungama. Badala yake, kwa kuwa ugonjwa wa kiroho unahusika, wazee wanapaswa kuchukua hatua ili ‘kumponya mtu huyo asiyejisikia vizuri.’ Kuna mambo mawili yaliyotajwa na Yakobo ambayo yanaweza kufanywa.
-
-
Je, Kuungama Dhambi Ni Takwa la Mungu?Mnara wa Mlinzi—2010 | Septemba 1
-
-
Kisha, anataja “sala ya imani.” Ingawa sala za wanaume wazee haziwezi kumfanya Mungu asifuate haki, sala hizo ni muhimu kwa Mungu, ambaye anatamani kusamehe dhambi kwa msingi wa fidia, au dhabihu ya ukombozi ya Kristo. (1 Yohana 2:2) Mungu yuko tayari kumsaidia mtenda dhambi yeyote anayetubu kikweli na anayefanya “matendo yanayostahili toba.”—Matendo 26:20.
-