Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je! Wewe Una Imani Kama Ile ya Eliya?
    Mnara wa Mlinzi—1992 | Aprili 1
    • Ebu wazia mwanamume huyo, amevaa vazi lake la kimashamba la singa. Yeye ni mwenyeji wa Giliadi yenye vilima-vilima vyenye kuchongoka, yaelekea alilelewa miongoni mwa wachungaji wa makundi wanyenyekevu. Asimama mbele ya Mfalme Ahabu mwenye nguvu, labda mle mle ndani ya makao yake makubwa mno ya kifalme, yakiwa na nyumba yayo yenye sifa sana ya pembe, mapambo yayo yenye kuvutia ajabu na sanamu kubwa mno. Humo, katika jiji lenye shamrashamra na lenye ngome la Samaria, ambamo ibada ya Yehova yakaribia sana kusahauliwa, amwambia Ahabu kwamba huyo mungu wake, huyo Baali, hana uwezo, huyo si kitu. Kwa mwaka huu, na kwa miaka ijayo, atangaza Eliya, hakutakuwa wala mvua wala umande!

      Yeye alipata wapi imani kama hiyo? Je! yeye hakuhisi woga, akisimama mbele ya huyo mfalme mwasi-imani, mwenye kiburi? Labda. Zaidi ya miaka elfu moja baadaye, ndugu nusu wa Yesu, Yakobo atuhakikishia kwamba Eliya alikuwa “mwanadamu mwenye tabia moja na sisi.” (Yakobo 5:17) Lakini angalia maneno ya Eliya: “Kama BWANA [YEHOVA, NW], Mungu wa Israeli ambaye ninasimama mbele zake aishivyo.” Eliya alikumbuka kwamba akiwa mtumishi wa Yehova, alikuwa anasimama mbele ya kiti cha ufalme kikubwa zaidi ya kile cha Ahabu—kiti cha ufalme cha Bwana Mwenye Enzi Kuu wa ulimwengu wote mzima! Alikuwa mwakilishi, mjumbe, wa hicho kiti cha ufalme. Akiwa na maoni hayo, alikuwa na nini cha kuogopa kutoka kwa Ahabu, mtawala duni wa kibinadamu ambaye alikuwa amepoteza baraka ya Yehova?

      Halikuwa tukio lisilotazamiwa kwamba Yehova alikuwa halisi sana hivyo kwa Eliya. Hakika nabii huyo alikuwa amejifunza juu ya shughuli za Yehova pamoja na watu Wake. Yehova alikuwa amewaonya Wayahudi kwamba angewaadhibu kwa ukame na njaa ikiwa wangegeuka na kuabudu miungu bandia. (Kumbukumbu la Torati 11:16, 17) Akiwa na uhakika kwamba sikuzote Yehova hutimiza neno lake, Eliya “akaomba kwa bidii mvua isinye.”—Yakobo 5:17.

  • Je! Wewe Una Imani Kama Ile ya Eliya?
    Mnara wa Mlinzi—1992 | Aprili 1
    • a Wote wawili Yesu na Yakobo husema kwamba haikunya mvua katika nchi kwa “miaka mitatu na miezi sita.” Hata hivyo, yasemekana kwamba Eliya alijitokeza mbele ya Ahabu mwishoni mwa ukame “katika mwaka wa tatu”—bila shaka kuhesabu tokea siku ile alipotangaza ukame. Hivyo, lazime iwe ilikuwa mwishoni mwa majira marefu ya ukame, usiyo na mvua wakati aliposimama mbele ya Ahabu kwa mara ya kwanza.—Luka 4:25; Yakobo 5:17; 1 Wafalme 18:1.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki