-
Jinsi ya Kudumisha Shangwe Tunapovumilia MajaribuMnara wa Mlinzi (Funzo)—2021 | Februari
-
-
2 Kwa kawaida, watu hawayaoni mateso kuwa sababu ya kuwa na shangwe. Lakini hivyo ndivyo Neno la Mungu linavyotuambia. Kwa mfano, mwanafunzi Yakobo aliandika kwamba badala ya kulemewa, tunapaswa kuona yote kuwa shangwe tunapopata majaribu. (Yak. 1:2, 12) Na Yesu alisema kwamba tunapaswa kuwa na furaha hata tunapoteswa. (Soma Mathayo 5:11.) Tunaweza kudumishaje shangwe yetu licha ya majaribu? Tunaweza kujifunza mambo mengi kwa kuchunguza mambo machache kutoka katika barua ambayo Yakobo aliwaandikia Wakristo wa mapema. Kwanza, acheni tuchunguze changamoto ambazo Wakristo hao walikabili.
WAKRISTO WA KARNE YA KWANZA WALIKABILI MAJARIBU GANI?
3. Ni nini kilitokea muda mfupi baada ya Yakobo kuwa mwanafunzi wa Yesu?
3 Muda mfupi baada ya Yakobo, ndugu nusu ya Yesu, kuwa mwanafunzi, upinzani ulizuka dhidi ya Wakristo huko Yerusalemu. (Mdo. 1:14; 5:17, 18) Na mwanafunzi Stefano alipouawa, Wakristo wengi walikimbia jiji hilo na “wakatawanyika kotekote katika maeneo ya Yudea na Samaria” na mwishowe wakafika maeneo ya mbali kama vile Kipro na Antiokia. (Mdo. 7:58–8:1; 11:19) Wanafunzi walikabili matatizo mengi sana. Hata hivyo, kwa bidii walihubiri habari njema popote walipoenda na makutaniko yakaanzishwa kotekote katika Milki ya Roma. (1 Pet. 1:1) Lakini baada ya hapo walipatwa na hali nyingi ngumu zaidi.
4. Wakristo wa mapema walihitaji kuvumilia majaribu gani mengine?
4 Wakristo wa mapema walihitaji kuvumilia majaribu mbalimbali. Kwa mfano, karibu mwaka wa 50 W.K., Maliki Mroma Klaudio aliamuru kwamba Wayahudi wote waondoke Roma. Hivyo, Wayahudi ambao walikuwa Wakristo, walilazimishwa kuyaacha makazi yao na kuhamia maeneo mengine. (Mdo. 18:1-3) Karibu mwaka wa 61 W.K., mtume Paulo aliandika kwamba Wakristo wenzake walishutumiwa hadharani, wakatupwa gerezani, na kuporwa mali zao. (Ebr. 10:32-34) Na kama tu ilivyokuwa kwa watu wengine, Wakristo walihitaji kuvumilia umaskini na magonjwa.—Rom. 15:26; Flp. 2:25-27.
-
-
Jinsi ya Kudumisha Shangwe Tunapovumilia MajaribuMnara wa Mlinzi (Funzo)—2021 | Februari
-
-
Kama mwale wa moto unaoendelea kuwaka ukiwa unalindwa ndani ya taa, ndivyo shangwe ambayo Yehova hutupatia inavyoendelea kuwaka ndani ya moyo wa Mkristo (Tazama fungu la 6)
6. Kulingana na Luka 6:22, 23, kwa nini Mkristo anaweza kuwa na shangwe anapokabili majaribu?
6 Huenda watu wakafikiri kwamba wanaweza kuwa na furaha ikiwa tu wana afya nzuri, wana pesa nyingi, na uhusiano wenye amani pamoja na washiriki wa familia. Lakini aina ya shangwe ambayo Yakobo aliandika kuhusu ni sehemu ya tunda la roho ya Mungu na haitegemei hali za mtu. (Gal. 5:22) Mkristo anapata shangwe au anakuwa na furaha ya kweli kwa kujua kwamba anampendeza Yehova na kufuata mfano wa Yesu. (Soma Luka 6:22, 23; Kol. 1:10, 11) Kama mwale wa moto unaolindwa ndani ya taa ya chemni (chemli), aina hii ya shangwe inawaka ndani ya moyo wa Mkristo. Haipungui tunapokuwa wagonjwa au tunapokuwa na pesa kidogo. Na haipotei tunapodhihakiwa au kupingwa na washiriki wa familia au watu wengine. Badala ya kuzima, taa yetu inazidi kuwaka hata zaidi kila mara wapinzani wanapojaribu kuizima. Majaribu tunayokabili kwa sababu ya imani yetu, yanathibitisha kwamba sisi ni wanafunzi wa kweli wa Kristo. (Mt. 10:22; 24:9; Yoh. 15:20) Hivyo, Yakobo alikuwa na sababu nzuri ya kuandika hivi: “Oneni yote kuwa shangwe, ndugu zangu, mnapopata majaribu mbalimbali.”—Yak. 1:2.
-