-
Shikamana na Tengenezo la YehovaTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
8 Umuhimu wa kusitawisha uvumilivu unakaziwa katika maneno haya yaliyoandikwa na Yakobo: “Oneni yote kuwa shangwe, ndugu zangu, mnapopata majaribu mbalimbali, mkijua kwamba sifa iliyojaribiwa ya imani yenu hutokeza uvumilivu. Lakini acheni uvumilivu ukamilishe kazi yake, ili muwe kamili na timamu katika mambo yote, bila kukosa kitu chochote.” (Yak. 1:2-4) Yakobo anasema kwamba Wakristo wanapaswa kuyakubali majaribu na kuyaona kuwa shangwe kwa sababu yanatusaidia kusitawisha uvumilivu. Je, hivyo ndivyo unavyoyaona majaribu? Kisha Yakobo anaonyesha kwamba uvumilivu wenyewe una kazi ya kufanya katika kukamilisha utu wetu wa Kikristo na kutufanya tuwe wenye kukubalika kabisa mbele za Mungu. Naam, uvumilivu wetu huongezeka siku baada ya siku tunapokabiliana na kushinda majaribu. Nao, uvumilivu hutokeza sifa nyingine zenye kupendeza tunazohitaji.
-
-
Shikamana na Tengenezo la YehovaTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
10 Ili tuendelee kuvumilia katika nyakati hizi ngumu, tunahitaji kuwa na maoni yanayofaa kuhusu kuteseka tukiwa Wakristo. Kumbuka kwamba Yakobo aliandika hivi: “Oneni yote kuwa shangwe.” Huenda isiwe rahisi kudumisha shangwe tunapoteseka kimwili au kiakili. Hata hivyo, kumbuka kwamba uhai wetu wa wakati ujao unahusika. Mfano wa mitume unatusaidia kuona jinsi tunavyoweza kushangilia tunapoteseka. Simulizi moja linapatikana katika kitabu cha Matendo, na linasema hivi: “Wakawaita mitume, wakawapiga viboko, na kuwaagiza waache kusema kwa msingi wa jina la Yesu, kisha wakawaacha waende. Basi wakatoka mbele ya Sanhedrini, wakishangilia kwa sababu walikuwa wamestahili kuvunjiwa heshima kwa ajili ya jina lake.” (Mdo. 5:40, 41) Walielewa kwamba mateso yao ni uthibitisho wa kwamba wanatii amri ya Yesu na kwamba wana kibali cha Yehova. Miaka kadhaa baadaye, alipokuwa akiandika barua yake ya kwanza iliyoongozwa na roho, Petro alitaja faida za kuteseka kwa ajili ya uadilifu.—1 Pet. 4:12-16.
-