Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Mashahidi wa Yehova ni Wakristo wa kweli?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 3. Mashahidi wa Yehova wanaigaje upendo wa Yesu?

      Yesu aliwapenda sana wanafunzi wake hivi kwamba walikuwa kama familia yake. (Soma Marko 3:35.) Vivyo hivyo, Mashahidi wa Yehova ni familia ya ulimwenguni pote yenye umoja. Ndiyo sababu tunaitana ndugu na dada. (Filemoni 1, 2) Vilevile tunatii amri hii: “Upendeni ushirika mzima wa akina ndugu.” (1 Petro 2:17) Mashahidi wa Yehova wanaonyesha upendo katika njia nyingi, kwa mfano, tunawasaidia waamini wenzetu ulimwenguni pote wanapohitaji msaada.

  • Ubatizo​—Lengo Muhimu!
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 6. Tunapobatizwa tunajiunga na familia ya Yehova

      Tunapobatizwa tunajiunga na familia yenye umoja ya ulimwenguni pote. Ingawa tumetoka katika maeneo na malezi mbalimbali, sisi sote tunaamini mambo yaleyale na tunaishi kulingana na viwango vilevile vya maadili. Soma Zaburi 25:14 na 1 Petro 2:17, kisha mzungumzie swali hili:

      • Mtu anapobatizwa anakuwa na uhusiano gani na Yehova na watu wengine wanaomwabudu?

      Picha: Dada aliyebatizwa akifikiria kuhusu uhusiano mzuri alio nao pamoja na wengine kutanikoni. 1. Anamweleza hisia zake dada fulani. 2. Anamsaidia dada aliyezeeka kutembea. 3. Anafurahia chakula pamoja na marafiki wenye umri mbalimbali. 4. Anamhubiria mwanamume akiwa pamoja na dada mwingine. 5. Anapiga picha na Mashahidi wawili kutoka jamii tofauti kwenye kusanyiko.
  • Dumisha Umoja Katika Kutaniko
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • Tunapokuwa pamoja na waabudu wenzetu, tunahisi kama Mfalme Daudi aliyesema hivi: “Jinsi ilivyo vema na jinsi inavyopendeza ndugu kukaa pamoja kwa umoja!” (Zaburi 133:1) Umoja wetu haujitokezi wenyewe. Kila mmoja wetu anachangia kudumisha umoja huo.

      1. Watu wa Mungu wana jambo gani la pekee?

      Unapohudhuria mkutano wa kutaniko katika nchi nyingine, huenda usielewe lugha inayozungumzwa, lakini utastarehe na kuhisi kwamba umekaribishwa. Kwa nini? Kwa sababu duniani pote tunajifunza Biblia kwa kutumia machapisho yaleyale. Na tunafanya yote tunayoweza ili kuonyeshana upendo. Hata iwe tunaishi wapi, sisi sote ‘tunaliitia jina la Yehova na kumwabudu kwa umoja.’​—Sefania 3:9, maelezo ya chini.

      2. Unaweza kufanya nini ili kuchangia umoja?

      “Pendaneni sana kutoka moyoni.” (1 Petro 1:22) Unawezaje kufuata ushauri huo? Badala ya kukazia fikira udhaifu wa wengine, kazia fikira sifa zao nzuri. Jitahidi kuwafahamu ndugu na dada wenye malezi mbalimbali badala ya kushirikiana tu na wale walio na mapendezi kama yako. Pia, tunapaswa kujitahidi kabisa kuondoa hisia zozote za ubaguzi ambazo huenda tunazo.​—Soma 1 Petro 2:17.a

      3. Utafanya nini hali ya kutoelewana ikitokea kati yako na Mkristo mwenzako?

      Ingawa tuna umoja, sisi si wakamilifu. Wakati fulani, tunaweza kuwavunja moyo waabudu wenzetu au kuwaumiza hisia. Kwa hiyo, Neno la Mungu linatuhimiza hivi: “Endeleeni . . . kusameheana,” kisha linaongeza hivi: “Kama vile Yehova alivyowasamehe kwa hiari, nanyi lazima mfanye vivyo hivyo.” (Soma Wakolosai 3:13.) Sisi humkosea Yehova mara nyingi sana, hata hivyo bado anatusamehe. Basi anataka tuwasamehe ndugu zetu. Ukigundua kwamba umemkosea mtu fulani, chukua hatua ya kwanza ili kusuluhisha tatizo hilo.​​—Soma Mathayo 5:​23, 24.b

      CHIMBA ZAIDI

      Chunguza njia unazoweza kuchangia umoja na amani katika kutaniko.

      Picha: Ndugu akifanya amani. 1. Ndugu mwingine anazungumza naye kwa hasira. 2. Anafikiria mambo ambayo ndugu huyo alisema. 3. Anachunguza ushauri wa Biblia kuhusu jinsi anavyopaswa kutenda anapokosewa. 4. Anakutana na yule ndugu, wanakunywa kahawa pamoja na kufanya amani.

      Utachukua hatua gani ili kufanya amani?

      4. Epuka ubaguzi

      Tunapaswa kuwapenda ndugu zetu wote. Lakini huenda ikawa vigumu kushirikiana na mtu ambaye tunamwona kuwa tofauti. Ni nini kitakachotusaidia? Soma Matendo 10:34, 35, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Yehova anakubali watu wa kila aina wawe Mashahidi wake. Unawezaje kuwa na maoni kama ya Yehova kuhusu watu walio na malezi tofauti na yako?

      • Ni ubaguzi wa aina gani ulio katika eneo lenu ambao ungependa kuepuka?

      Soma 2 Wakorintho 6:11-13, kisha mzungumzie swali hili:

      • Unawezaje kuimarisha upendo kati yako na ndugu na dada walio na malezi tofauti na yako?

      5. Samehe kwa hiari na ufanye amani

      Yehova hutusamehe kwa hiari ingawa yeye hahitaji kamwe sisi tumsamehe. Soma Zaburi 86:5, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Yehova husamehe kwa njia kubwa jinsi gani?

      • Kwa nini unathamini msamaha wake?

      • Ni hali gani zinazoweza kusababisha kutoelewana kati yetu na watu wengine?

      Tunawezaje kumwiga Yehova na kuendelea kushirikiana na ndugu na dada zetu kwa umoja? Soma Methali 19:11, kisha mzungumzie swali hili:

      • Mtu anapofanya jambo linalokuudhi au kukukasirisha, unaweza kufanya nini ili kusuluhisha hali hiyo?

      Wakati fulani sisi huwakosea wengine. Unapaswa kufanya nini hilo linapotokea? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

      VIDEO: Kufanya Amani Huleta Baraka (6:01)

      • Katika video hiyo, dada huyo alichukua hatua gani ili kufanya amani?

      6. Kazia fikira sifa nzuri za ndugu na dada zako

      Tunapozidi kuwafahamu ndugu na dada zetu, tunatambua sifa zao nzuri na pia udhaifu wao. Tunawezaje kukazia fikira sifa zao nzuri? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

      VIDEO: Boresha Utu Wako wa Kikristo! (5:10)

      • Ni nini kinachoweza kukusaidia kuona sifa nzuri za ndugu na dada zako?

      Yehova hukazia fikira sifa zetu nzuri. Soma 2 Mambo ya Nyakati 16:9a, kisha mzungumzie swali hili:

      • Unahisije kujua kwamba Yehova anakazia fikira sifa zako nzuri?

      Pete ya almasi.

      Hata almasi maridadi ina kasoro lakini bado ni yenye thamani. Vivyo hivyo, ndugu na dada zetu wote si wakamilifu, lakini ni wenye thamani mbele za Yehova

      WATU FULANI HUSEMA: “Ili nimsamehe mtu, lazima kwanza aniombe msamaha.”

      • Kwa nini tunapaswa kuwa tayari kuwasamehe wengine?

      MUHTASARI

      Unaweza kudumisha umoja kutanikoni kwa kuwasamehe na kuwapenda ndugu na dada zako wote.

      Ungejibuje?

      • Unawezaje kuepuka ubaguzi?

      • Utafanya nini hali ya kutoelewana ikitokea kati yako na Mkristo mwenzako?

      • Kwa nini unapaswa kuiga mfano wa Yehova wa kuwasamehe wengine?

      Lengo

      CHUNGUZA ZAIDI

      Jifunze jinsi mfano ambao Yesu alitoa unavyoweza kutusaidia kuepuka kuwahukumu wengine.

      Toa Boriti (7:01)

      Je, tunahitaji kuomba msamaha hata ikiwa tunahisi kwamba hatujakosea?

      “Kuomba Msamaha​—Ni Njia Bora ya Kufanya Amani” (Mnara wa Mlinzi, Novemba 1, 2002)

      Ona jinsi wengine walivyojifunza kuacha kuwabagua wengine..

      Usihukumu Kwa Sura ya Nje (5:06)

      Jifunze jinsi ya kutatua hali ya kutoelewana kati yako na Mkristo mwenzako kabla haijavuruga amani kutanikoni.

      “Suluhisha kwa Upendo Hali ya Kutoelewana” (Mnara wa Mlinzi, Mei 2016)

      a Maelezo ya Ziada 6 yanazungumzia jinsi upendo unavyowachochea Wakristo waepuke kueneza magonjwa yanayoambukiza.

      b Maelezo ya Ziada 7 yanazungumzia jinsi ya kusuluhisha matatizo ya kibiashara na kisheria.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki