Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Akawasikitikia”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • Picha katika ukurasa wa 154

      Onyesha “hisia-mwenzi”

      7. Ni nini kinachoweza kutusaidia kusitawisha sifa ya kuelewa hisia za wengine, nasi tunaweza kuonyesha sifa hiyo jinsi gani?

      7 Tukiwa Wakristo, tunatiwa moyo kumwiga Yesu kwa kuelewa hisia za wengine. Biblia inatusihi tuwe na “hisia-mwenzi.”b (1 Petro 3:8) Huenda isiwe rahisi kuelewa hisia za wale wanaougua magonjwa ya kudumu au walioshuka moyo sana, hasa ikiwa sisi wenyewe hatujawahi kupatwa na maumivu hayo. Lakini, kumbuka kwamba si lazima mtu awe amepatwa na mambo ambayo yamewapata wengine ili aelewe jinsi wanavyohisi. Yesu alielewa hisia za wagonjwa hata ingawa yeye mwenyewe hakupata kuwa mgonjwa. Hivyo basi, tunaweza kusitawisha namna gani sifa ya kuelewa hisia za wengine? Kwa kusikiliza kwa subira wale wanaoteseka wanapotueleza matatizo yao na hisia zao. Tunaweza kujiuliza, ‘Ikiwa ningekabili hali kama yao, ningehisi namna gani?’ (1 Wakorintho 12:26) Tukijitahidi kuhisi jinsi wengine wanavyohisi, itakuwa rahisi zaidi “kuzifariji nafsi zilizohuzunika.” (1 Wathesalonike 5:14) Nyakati nyingine, tunaweza kuonyesha kwamba tunaelewa jinsi wengine wanavyohisi si kwa maneno yetu tu bali hata kwa machozi. Andiko la Waroma 12:15 linasema: “Lieni pamoja na watu wanaolia.”

  • “Akawasikitikia”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • b Neno la Kigiriki linalotafsiriwa “hisia-mwenzi” linamaanisha “kuteseka pamoja na.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki