-
‘Yule Mtumwa Mwaminifu’ Apita Mtihani wa Ukaguzi!Mnara wa Mlinzi—2004 | Machi 1
-
-
15, 16. (a) Wakati wa kufanya hesabu ulifika lini? (b) Ni nafasi gani mpya za “kufanya biashara” ambazo wale walio waaminifu walipewa?
15 Katika mfano huo Yesu anaendelea kusema: “Baada ya muda mrefu bwana wa watumwa hao alikuja na kufanya hesabu pamoja nao.” (Mathayo 25:19) Katika mwaka wa 1914—bila shaka muda mrefu baada ya 33 W.K.—kuwapo kwa Kristo Yesu akiwa mfalme kulianza. Mnamo mwaka wa 1918, miaka mitatu na nusu baadaye, alikuja kwenye hekalu la Mungu la kiroho na kutimiza maneno haya ya Petro: “Ni wakati uliowekwa wa hukumu kuanza na nyumba ya Mungu.” (1 Petro 4:17; Malaki 3:1) Ulikuwa wakati wa kufanya hesabu.
-
-
‘Yule Mtumwa Mwaminifu’ Apita Mtihani wa Ukaguzi!Mnara wa Mlinzi—2004 | Machi 1
-
-
Mathayo sura ya 24 na ya 25, husema kwamba Yesu ‘angekuja’ katika maana mbalimbali. Ili “kuja,” Yesu hahitaji kuondoka mahali fulani na kwenda mahali pengine. Badala yake ‘anakuja’ katika maana ya kuelekeza fikira zake kwa wanadamu au kwa wafuasi wake, mara nyingi ili kuwahukumu. Hivyo, mnamo mwaka wa 1914 ‘alikuja’ ili kuwapo kwake kuanze akiwa Mfalme aliyetawazwa. (Mathayo 16:28; 17:1; Matendo 1:11) Katika mwaka wa 1918 ‘alikuja’ akiwa mjumbe wa agano na kuanza kuwahukumu wale waliodai kumtumikia Yehova. (Malaki 3:1-3; 1 Petro 4:17) Kwenye Har-magedoni, ‘atakuja’ ili kuwahukumu maadui wa Yehova.—Ufunuo 19:11-16.
-