-
“Wachungaji Wenye Kupatana na Moyo Wangu”Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
-
-
4. Ni nani wanaowatunza kondoo wa Mungu leo, nao wanafanya hivyo wakiwa na roho gani?
4 Ahadi ya Mungu ilitimizwa kwa kiwango kikubwa na yule Mchungaji Mkuu wa kondoo za Yehova, Yesu, ambaye ndiye Kichwa cha kutaniko la Kikristo. Alijiita mwenyewe “mchungaji mwema,” anayewahurumia kikweli wale walio chini ya uongozi wake. (Yoh. 10:11-15) Leo, Yehova anawatumia wachungaji, walio chini ya uongozi wa Yesu, kuwatunza kondoo wake hapa duniani. Wachungaji hao ni ndugu watiwa-mafuta wa jamii ya mtumwa mwaminifu na mwenye busara na pia wazee wenye bidii wa “umati mkubwa.” (Ufu. 7:9) Ndugu hao hujitahidi kuonyesha roho ya kujidhabihu kama Yesu alivyofanya. Wanamwiga Kristo kwa kulithamini na kulilisha kutaniko. Ole kwa wowote ambao wanawapuuza au wanaopiga ubwana juu ya ndugu zao au ambao wanawatendea kwa ukali au kiburi! (Mt. 20:25-27; 1 Pet. 5:2, 3) Yehova anatazamia wachungaji Wakristo leo watimize nini? Tunaweza kujifunza nini kutokana na yale ambayo Yeremia aliandika kuhusu mtazamo unaofaa na lengo ambalo wazee wanapaswa kuwa nalo wanapoendelea kutekeleza majukumu yao? Acheni tuchunguze majukumu yao ya kutoa msaada na ulinzi, ya kufundisha ndani na nje ya kutaniko, na ya kutoa hukumu.
-
-
“Wachungaji Wenye Kupatana na Moyo Wangu”Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
-
-
6 Kama wachungaji halisi, waangalizi Wakristo hawapaswi kulitunza kutaniko kwa uzembe. Ikiwa wewe ni mzee wa kutaniko, je, unajitahidi kuwa macho kuona dalili yoyote ya kwamba ndugu zako wana mahangaiko na je, uko tayari kutoa msaada haraka? Mfalme mwenye hekima Sulemani alisema hivi: “Unapaswa kujua vizuri hali ya kundi lako. Elekeza moyo wako kwenye makundi yako.” (Met. 27:23) Mstari huo unazungumzia bidii ya mchungaji halisi, hata hivyo, kanuni yenyewe inaweza kutumiwa kuhusiana na kazi ya wachungaji wa kiroho katika kutaniko. Ikiwa wewe ni mzee wa kutaniko, je, unaepuka mwelekeo wa kupiga ubwana juu ya wengine? Maneno ya Petro kuhusu “kupiga ubwana juu ya wale ambao ni urithi wa Mungu” yanaonyesha kwamba kuna uwezekano wa kufanya hivyo. Unaweza kushiriki jinsi gani katika utimizo wa maneno ya Yeremia 33:12? (Soma.) Wazazi wasio na mwenzi, wajane, familia za kambo, wazee kwa umri, na vijana huenda wakahitaji ufikirio na msaada wa pekee.
-