-
Ninataka Kufa—Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Ikiwa Nina Mawazo ya Kujiua?Maswali ya Biblia Yajibiwa
-
-
Biblia inasema hivi: ‘Mtupieni Mungu mahangaiko yenu yote, kwa sababu yeye anawajali ninyi.’—1 Petro 5:7.
Maana: Mungu anakukaribisha umweleze waziwazi na kwa unyoofu kuhusu chochote kinachokuhangaisha.
Mungu anaweza kukupa amani ya akili na nguvu za kuendelea kuvumilia hali yako. (Wafilipi 4:6, 7, 13) Kwa njia hiyo, yeye huwategemeza wale wanaomwomba msaada.—Zaburi 55:22.
-