-
Itikia Ahadi za Mungu kwa Kuzoea ImaniMnara wa Mlinzi—1993 | Julai 15
-
-
4. Tunapaswa kutia sifa zipi katika imani yetu?
4 Imani katika ahadi za Yehova na shukrani kwa ajili ya uhuru wetu wenye kupewa na Mungu yapaswa kutusukuma tujitahidi kadiri tuwezavyo kuwa Wakristo wenye kielelezo kizuri. Petro alisema hivi: “Mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema [wema-adili, NW], na katika wema wenu maarifa [ujuzi, NW], na katika maarifa yenu kiasi [kujidhibiti, NW], na katika kiasi chenu saburi [uvumilivu, NW], na katika saburi yenu utauwa [ujitoaji kimungu, NW], na katika utauwa wenu upendano wa ndugu [shauku ya kidugu, NW], na katika upendano wa ndugu, upendo.” (2 Petro 1:5-7) Hivyo Petro atutolea orodha ambayo ingefaa tuikariri. Acheni tuzichunguze sifa hizo kwa uangalifu zaidi.
-
-
Itikia Ahadi za Mungu kwa Kuzoea ImaniMnara wa Mlinzi—1993 | Julai 15
-
-
8. Kujidhibiti ni nini, nako kunahusianaje na uvumilivu?
8 Ili tuweze kukabili majaribu kwa imani, tunahitaji kutia katika ujuzi wetu kujidhibiti. Neno la Kigiriki kwa “kujidhibiti” laonyesha uwezo wa kujiweza wenyewe. Tunda hilo la roho ya Mungu hutusaidia tuonyeshe kujizuia katika wazo, neno, na mwenendo. Kwa udumifu katika kuzoea kujidhibiti, tunatia uvumilivu ndani yako. Neno la Kigiriki kwa “uvumilivu” lamaanisha uthabiti wenye ujasiri, si kukata tamaa kwa huzuni kwa sababu ya ugumu usioepukika. Ni kwa ajili ya shangwe iliyowekwa mbele yake kwamba Yesu alivumilia mti wa mateso. (Waebrania 12:2) Nguvu za kupewa na Mungu zinazoshirikishwa na uvumilivu huimarisha imani yetu na kutusaidia tushangilie katika dhiki, tukinze kishawishi, na kuepuka kuridhiana tunaponyanyaswa.—Wafilipi 4:13.
9. (a) Ujitoaji kimungu ni nini? (b) Kwa nini tutie shauku ya kidugu katika ujitoaji kimungu wetu? (c) Tunaweza kutiaje upendo katika shauku yetu ya kidugu?
9 Kwa uvumilivu wetu ni lazima tutie ujitoaji kimungu—kicho, ibada, na utumishi kwa Yehova. Imani yetu hukua tunapozoea ujitoaji kimungu na kuona jinsi Yehova anavyoshughulika na watu wake. Lakini, ili kuonyesha sifa ya kumcha Mungu, tunahitaji shauku ya kidugu. Kwani, “asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona.” (1 Yohana 4:20) Mioyo yetu yapasa itusukume tuonyeshe shauku ya kweli kwa watumishi wengine wa Yehova na kutafuta hali yao njema nyakati zote. (Yakobo 2:14-17) Lakini kwa nini tunaambiwa tutie upendo katika shauku yetu ya kidugu? Kwa wazi Petro alimaanisha kwamba ni lazima tuonyeshe upendo kwa ainabinadamu yote, si kwa ndugu zetu tu. Upendo huo unaonyeshwa hasa kwa kuhubiri habari njema na kuwasaidia watu kiroho.—Mathayo 24:14; 28:19, 20.
-