-
Mungu Aliipuliziaje Biblia?Mnara wa Mlinzi—1997 | Juni 15
-
-
Ikiwa hayakufunuliwa moja kwa moja na Mungu kwa mwandikaji, Mungu aliyajulisha matukio hayo kwa mtu fulani hivyo, hayo yakawa sehemu ya historia ya mdomo au iliyoandikwa, ambayo ilipitishwa kutoka kizazi kimoja hadi kilichofuata hadi yakawa sehemu ya rekodi ya Biblia. (Ona sanduku ukurasa wa 7.) Kwa vyovyote, twaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova ndiye aliyekuwa Chanzo cha habari hiyo yote, na aliwaongoza waandikaji hivi kwamba masimulizi yao hayakutiwa doa na mambo yasiyo sahihi, utiaji chumvi, au ngano. Petro aliandika hivi kuhusu unabii: “Wanadamu walisema kutoka kwa Mungu walipokuwa wakichukuliwa na roho takatifu.”b—2 Petro 1:21.
-
-
Mungu Aliipuliziaje Biblia?Mnara wa Mlinzi—1997 | Juni 15
-
-
b Neno la Kigiriki linalotafsiriwa hapa “wakichukuliwa,” pheʹro, linatumiwa katika njia nyingine kwenye Matendo 27:15, 17 ili kufafanua meli inayochukuliwa na upepo. Hivyo roho takatifu ‘iliongoza mwendo wa’ waandikaji wa Biblia. Iliwasukuma kukataa habari yoyote iliyokuwa ya uwongo na kutia ndani tu ile iliyokuwa ya hakika.
-