-
Onyesha Shukrani kwa Mambo Ambayo Yehova na Yesu WamekufanyiaFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
3. Tunaonyesha shukrani kupitia matendo
Wazia kwamba mtu fulani alikuokoa ili usizame ndani ya maji. Je, unaweza kusahau jambo ambalo mtu huyo alikufanyia? Au je, utatafuta njia za kumwonyesha shukrani kwa jambo alilokufanyia?
Yehova ndiye chanzo cha uhai wetu. Soma 1 Yohana 4:8-10, kisha mzungumzie maswali haya:
Kwa nini dhabihu ya Yesu ni zawadi ya pekee?
Unahisije kuhusu mambo ambayo Yehova na Yesu wamekufanyia?
Tunaweza kuonyeshaje shukrani kwa mambo ambayo Yehova na Yesu wametufanyia? Soma 2 Wakorintho 5:15 na 1 Yohana 4:11; 5:3. Baada ya kusoma kila andiko, zungumzieni swali hili:
Kulingana na andiko hilo, tunawezaje kuonyesha shukrani?
-
-
Kwa Nini Unapaswa Kujiweka Wakfu na Kubatizwa?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
1. Ni nini ambacho humchochea mtu ajiweke wakfu?
Tunachochewa na upendo kujiweka wakfu kwa Yehova. (1 Yohana 4:10, 19) Biblia inatuhimiza hivi: “[Mpende] Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.” (Marko 12:30) Tunaonyesha kwamba tunampenda Mungu si kwa maneno tu, bali pia kwa matendo yetu. Kama vile mwanamume na mwanamke wanaopendana sana wanavyoamua kufunga ndoa, vivyo hivyo kumpenda Yehova hutuchochea kujiweka wakfu kwake na kubatizwa.
-