-
Biblia Iliokoka Jitihada za Kubadili Ujumbe WakeMnara wa Mlinzi (Toleo la Watu wote)—2016 | Na. 4
-
-
Fundisho la Utatu: Miaka 300 hivi baada ya Biblia kuandikwa, mwandishi wa fundisho la Utatu aliongezea maneno haya katika andiko la 1 Yohana 5:7 “mbinguni, Baba, na Neno, na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja.” Maneno hayo hayakupatikana katika maandishi ya awali. Msomi wa Biblia Bruce Metzger anasema hivi: “Kuanzia karne ya sita na kuendelea, maneno hayo yalipatikana mara nyingi zaidi kwenye hati za Kilatini cha Zamani na Vulgate ya Kilatini.”
-
-
Biblia Iliokoka Jitihada za Kubadili Ujumbe WakeMnara wa Mlinzi (Toleo la Watu wote)—2016 | Na. 4
-
-
Pili, kwa kuwa hati nyingi za kale zinapatikana leo, wasomi wa Biblia wanaweza kutambua makosa kwa njia rahisi. Kwa mfano, kwa miaka mingi viongozi wa dini walifundisha kwamba tafsiri ya Biblia yao ya Kilatini ilikuwa sahihi. Hata hivyo, kama ilivyotajwa mwanzoni mwa makala hii waliongeza maneno yasiyo sahihi katika 1 Yohana 5:7. Makosa hayo yaliandikwa pia katika tafsiri ya Kiingereza ya King James Version! Hata hivyo, hati nyingine za kale zilizogunduliwa zilionyesha nini? Bruce Metzger aliandika: “Maneno [yaliyo kwenye 1 Yohana 5:7] hayapatikani kwenye hati zote za awali (Kisiria, Kikoptiki, Kiarmenia, Kiethiopia, Kiarabu, Kislavonia) isipokuwa kwenye tafsiri ya Kilatini pekee.” Kwa sababu hiyo, tafsiri zilizoboreshwa za King James Version na Biblia nyingine zimeondoa fungu hilo la maneno lisilo sahihi.
-