-
Endelea Kutembea Katika Nuru ya KimunguMnara wa Mlinzi—1986 | Julai 15
-
-
8, 9. (a) Ni kwa msingi gani Yehova atatusamehe sisi? (b) Kwa habari ya dhambi, waasi-imani fulani walikuwa wakisema nini, na kwa sababu gani walikuwa wakikosea?
8 Halafu sasa Yohana anautaja msingi wa kusafishwa kutoka kwenye dhambi. (Soma 1 Yohana 1:8–2:2, NW.) Tikisema “sisi hatuna dhambi,” tunaukana uhakika wa kwamba wanadamu wote wasio wakamilifu ni wenye dhambi, na “ukweli haumo ndani yetu.” (Warumi 5:12) Lakini Mungu ni “mwaminifu” naye anatusamehe “ikiwa tunaungama dhambi zetu” kwake tukiwa na mwelekeo wa kutubu unaotusukuma tuache makosa. (Mithali 28:13) Mungu alisema hivi juu ya wale walio katika agano jipya: “Dhambi yao sitaikumbuka tena.” (Yeremia 31:31-34; Waebrania 8:7-12) Katika kuwasamehe wao, yeye ni mwaminifu kwa ahadi hiyo.
-
-
Endelea Kutembea Katika Nuru ya KimunguMnara wa Mlinzi—1986 | Julai 15
-
-
10. Ni kwa njia gani Yesu ni “dhabihu ya upatanisho”?
10 Yohana anaandika “mambo hayo” juu ya dhambi, msamaha, na kusafishwa ili sisi tusije tukazoea dhambi. Maneno yake yanapasa kutusukuma tujitahidi kwa bidii nyingi tusitende dhambi. (1 Wakorintho 15:34) Lakini tukitenda “dhambi” na kuwa wenye kutubu, tuna “msaidiaji pamoja na Baba”—“Yesu Kristo, mtu mwadilifu,” anayetetea mambo yetu kwa Mungu. (Waebrania 7:26, NW; Linganisha Yohana 17:9, 15, 20.) Yesu ni “dhabihu ya upatanisho.” Kifo chake kilitimiliza haki na kufanya iwezekane Mungu atuonyoshe rehema na kuliondoa shtaka la dhambi kwa habari ya Waisraeli wa kiroho na ‘ulimwengu mzima,’ kutia na ule “mkutano mkubwa” (Ufunuo 7:4-14; Warumi 6:23; Wagalatia 6:16) Sisi tunaithamini dhabihu yake kama nini!
-