-
Inamaanisha Nini Kutounga Mkono Upande WowoteFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
2. Tunawezaje kuonyesha kwamba hatuungi mkono upande wowote?
Kama Yesu, sisi pia hatujihusishi na siasa. Watu walipoona muujiza mmoja wa Yesu, walitaka kumfanya awe Mfalme wao duniani, lakini alikataa. (Yohana 6:15) Kwa nini alikataa? Kwa sababu baadaye alisema hivi: “Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu.” (Yohana 18:36) Tukiwa wanafunzi wa Yesu, tunaonyesha kwa njia mbalimbali kwamba hatuungi mkono upande wowote. Kwa mfano, hatushiriki katika vita. (Soma Mika 4:3.) Tunaheshimu nembo za taifa kama vile bendera, lakini hatuziabudu. (1 Yohana 5:21) Na hatuungi mkono wala kupinga mgombeaji au chama chochote cha kisiasa. Kwa kufanya hivyo, tunaonyesha kwamba sisi ni washikamanifu kabisa kwa serikali ya Mungu, yaani, Ufalme wake.
-
-
Inamaanisha Nini Kutounga Mkono Upande WowoteFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
4. Onyesha kwamba huungi mkono upande wowote kupitia mawazo na matendo yako
Soma 1 Yohana 5:21. Kisha, onyesha VIDEO na mzungumzie maswali yanayofuata.
Katika video hiyo, kwa nini Ayenge alikataa kujiunga na chama cha kisiasa au kushiriki katika sherehe za kitaifa, kama vile kupiga saluti mbele ya bendera?
Je, unafikiri alifanya uamuzi wa hekima?
Msimamo wetu wa kutounga mkono upande wowote unaweza kujaribiwa katika hali gani nyingine? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.
Tunawezaje kuonyesha kwamba hatuungi mkono upande wowote kunapokuwa na mashindano ya michezo kati ya mataifa mbalimbali?
Tunawezaje kuendelea kutounga mkono upande wowote, iwe maamuzi ya wanasiasa yatatunufaisha au kutuletea madhara?
Msimamo wetu wa kutounga mkono upande wowote unawezaje kuathiriwa na mambo tunayosikia katika vyombo vya habari au watu tunaoshirikiana nao?
Ni katika hali gani ambazo Mkristo anapaswa kudumisha msimamo wa kutounga mkono upande wowote kupitia mawazo na matendo yake?
-